ads

Tuesday 21 November 2023

BASI













Kaditama nimetua, sisongi sirudi tena,
Mambo nimeyatibua, hata nife hutoguna,
Kweli yote nimejua, ulianza mbali sana,
Basi.
Nilihisi tunaota, kumbe ninajidanganya,
Ilipita myaka sita, sina nililolifanya,
Mwenyewe ukajipata, mwenyewe sikujiponya,
Basi.
Nikaiweka busara, kumbe linaletwa shari,
Kaona kovu imara, kumbe njia ya hatari,
Ninazuia hasira, waniotea kaburi,
Basi.
Kaniundia ubaya, kwote wanone kituko,
Kutwa naijenga kaya, mwenzangu kucha mitoko,
Kila siku kwangu mbaya, kumbe kwako ni ujiko,
Basi.
Kihisi yule adui, kwake utajibagaza,
Nikajifanya sijui, sije wana waumiza,
Nilishajua wewe chui, heri kwangu kunyamaza,
Basi.
Niliposaka suluhu, wapasha vyako viporo,
Kavuka hadi Ruhuhu, Pwani hadi Morogoro,
Kumbe umeshakubuhu, mie kunipa kasoro,
Basi.
Umeutibua moyo, akili na wangu mwili,
Heri un'one na choyo, naipamba yangu hali,
Sasa ninatoka mbiyo, nikusanye zangu mali,
Basi.
Basi sasa imetosha, yote nimeyakubali,
Basi sasa yamekwisha, sasa ninakwenda mbali,
Basi sitokukumbusha, zile ahadi za kweli,

Basi. 

KAMA NINGEKUWA JUA













Huwa halioni wivu, wala kuchukia kitu,
Jua halina uchovu, halibadiliki katu,
Huwa linatunza nguvu, jua si kama msitu,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Jua shahidi wa vingi, wala haliji kusema,
Usiri kwake msingi, halijawahi kugoma,
Iwe mboga iwe bangi, moja hawezi kuchoma,
Heri ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Singetamani usiku, wote mkawa nuruni,
Na nikasirike siku, niwache wiki gizani,
Wacha munone kasuku, mkanitoa thamani,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Mngeona tabasamu, hata nikiwa tabuni,
Mkininyima salamu, isinifike moyoni,
Hata nisiwaze simu, anayepiga ni nani,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Nizipuuze ahadi, mliziweka gizani,
Nisipandishe midadi, mkikana hararani,
Ama kumwona hasidi, akitamba kanisani,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Ugonjwa ningepuuza, na kuikwepa sonona,
Hili linalonunguza, nisingelijali sana,
Kimya ningejiuguza, nikafa hata kupona,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Ningekuwa peke yangu, mwezi na wingu kwa mbali,
Nisingewaza uchungu, nyota siponikubali,
Zaidi ni wangu Mungu, langu pendo astahili,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Singekuwa na wana, nife wakanililia,
Na mke tukagombana, ili aje nikimbia,
Wala kusema hapana, nishindwe kuvumilia,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Nisingemuwaza mama, au baba kumjali,
Huko na huko kusoma, kisha nife kwa ajali,
Mama akashika tama, kuwazia yangu hali,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Basi hivyo siyo jua, siyo mvua wala nyota,
Macho nitayakodoa, na kusota nitasota,
Nikiumwa naumia, na furaha pia napata,
Kama ningekuwa jua.....

SIKU ZA UJANA WA DIEGO COSTA












Na. Kenny Anjelina

Aliamua kuacha starehe zote za nchini Brazil. Diego Costa the trouble some, akaacha pombe na bata za mitaa ya Rio de Janeiro na Santos.
Akaacha warembo wa fukwe za huko Brazil ambao huzurura na bikini huku wakinywa wine.
Akaicha nchi yake ya Brazil, akaliacha soka murua la samba akanunua uraia wa nchi ya Uhispania. Wahispaniola wakampokea, wakampa jezi namba 19. Wakamuimba kwenye Euro, wakamuimba kwenye Olimpiki, wakamuimba kwenye World Cup.
Mtukutu Diego Costa alikuwa mtu bhana. Wakati akiwa na jezi ya Chelsea na Atletico De Madrid alikuchezea kwanza rafu afu anaweka kwenye kamba. Hakuwa mlaini kama Olmo wa Uhispania ya leo.
Mwaka 2014 Mtukutu Diego Costa alisafiri na timu ya taifa ya Uhispania hadi Brazil kwenye mashindano ya kombe la dunia. Na ndo huko hadithi yangu inaanza.
Uhispania, Chille, Uholanzi na Australia walipangwa kundi 1. Wabrazil wakawa wanaomba Mungu Mtukufu Diego Costa na Hispania yake watolewe kwani wangetukanwa matusi mengi kutoka kwa Costa. Waliogopa kebehi za Costa kutwaa taji kwenye ardhi ya Brazil.
Mechi ya kwanza Spain wakapigwa 5-1 mbele ya Uholanzi. Shukrani kwa Van Persie na the killer Arjen Roben. Mechi ya pili Spain akafa 2-0 mbele ya Chille ya Vidal na Alexis Sanchez.
Hadi hapo Spain wakawa wametolewa. Hadithi ikawa fupi kwa the trouble some Diego Costa.
Wakati anatoka uwanjani wabrazil wakaanza kumzomea huku wakiimba "Adias spana! Adias Amigo!" Yaani kwaheri Rafiki kwaheri mwenzetu. Wabrazil wakanywa pombe na kufurahi usiku ule.

HAPO ZAMANI ZA KALE  

JINSI AMBAVYO RAIOLA ANGEISUMBUA DUNIA KWA MBAPPE












Na. Kenny Anjelina
April 30, 2022 juu ya kitanda kimoja kwenye hospitali ya San Raffaele nchini Italia, Mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 54, alikuwa anavuta pumzi ya mwisho.
Huyu alikuwa ni Mino Raiola, mzee wa fix, mzee wa kuchezesha miamala. Dalali na huni la kimataifa.
Mino Raiola alikuwa wakala wa Haland, Ibrahimovic, Pogba, na wengine wengi. Manchester United hawataki kabisa kumsikia.
Mino alikuwa na nguvu haswa na kazi yake aliifanya kisomi kwelikweli.
Jana, Mbappe amefikisha magoli 300. Nawaza kama Raiola angekuwa hai halafu awe wakala wa Mbappe. Nafikiri vilabu vingi Ulaya vingekaa kwa adabu. Sio PSG siyo Real Madrid, wala Barcelona.
Kwanza angeenda Sky Sports na kusema, "PSG ni timu kubwa, lakini tupo tayari kwa changamoto mpya. Kuna ofa nyingi mezani na tunazifanyia kazi. Lakini kwasasa ni mchezaji wa PSG na anafuraha ".
Hapo PSG wangehaha, kusikia hivyo wangepanga noti nyingi kumshawishi Mbappe aongeze mkataba.
Jumatano, angeenda kwenye gazeti la THE MIRROR na kusema, "Real Madrid ni klabu kubwa na ni ndoto ya kila mchezaji mkubwa. Tunawasikiliza Madrid wanasemaje " Hapo Perez angekunjua noti na kukaa mkao wa kula.
Jumamosi, angeenda THE SUN na kusema, "Jumatatu tutakutana na wawalilishi wa Manchester United kuhusu uhamisho wa Kylian. Ni kijana mdogo ambaye juzi amefikisha magoli 300. Lazima thamani yake iwe kubwa "
Kwahiyo kwa wiki moja tu tayari angewachonganisha PSG, Real Madrid na Manchester United. Ila sasa kumepoa sana.
Haland alitakiwa na Real Madrid wakati akiwa Salzburg. Lakini yeye akampitisha kwenye vituo vingi vya Dortmund na Manchester City ili apige pesa ya udalali mwote humo kabla ya kwenda Madrid au Barcelona. Mino ni Msela haswa.
Kwa vurugu zake na umaarufu wake, angepiga Pauni Milioni 25 pekee yake kwenye dili la Mbappe kwenda Madrid au kwingineko.
Kisha angechukua boti na kwenda kupumzika kwenye fukwe za Venezia akiwa tumbo wazi na mvinyo na warembo pembeni.
RIP RAIOLA

 

KIBURI KINAVYOWAUA WAJERUMANI














Na. Kenny Anjelina

Waingereza wanamsemo wao, Curiosity killed a cat. Yaani udadisi mwingi ulimuua paka. Paka hudadisi hata vitu vinavyomzidi uwezo mwisho hupata madhara na hata kufa.

July 13, 2014, usiku ule Wajerumani walikuwa na furaha sana. Unajua kwanini? Walikuwa wanatwaa taji la Kombe la Dunia, tena njiani wakitoka kutoa semina elekezi kwa Brazil, palepale kwao waliwapa 1-7. Raha iliyoje?

Nafikiri usiku ule pale Rio de Janeiro ndo tulimaliza ubora wa Ujerumani. Tangu hapo hatujaona hata robo ya mafanikio ya ubora wa Ujerumani ile.

Mwaka 2018 waliishia hatua ya makundi pale kwa Vladimir. Walishindwa kufurukuta mbele ya Korea kusini na wahuni Mexico. Bingwa mtetezi, akatolewa hatua ya makundi.

Watu wa mpira walihisi ni bahati mbaya tu. Lakini kilichojirudia mwaka 2022, pale Qatar, kutolewa tena kwenye makundi tukajua tu Ujerumani imeanguka.

Dunia nzima inajua Ujerumani imeisha lakini wao tu pekee ndo hawaamini kama wameisha. Wana kiburi, ndo kinachowaua.

Baada ya Qatar, wakacheza mechi nyingi ambazo zinawapalia kila siku. Lakini hawataki kuanza upya, wanaamini wao bado wapo timamu.

Mpira umebadilika, umetoka kwenye matumizi ya nguvu na kucheza kwa nafasi hadi kwenye matumizi ya sayansi ya mchezo na kutimiza majukumu ya pamoja.

Uingereza, Ufaransa na Uholanzi wapo huko. Argentina ndo tusiseme, unaona jinsi Rodrigo De Paul anavyohaha uwanja mzima. Hakuna matozi tena.

Ila Ujerumani wao bado wanaamini katika nguvu na kupishana. Bahati mbaya wana Gundogan na Musiala ambao hawawezi kutumia mabavu.

Juzi walijaribu kuacha kiburi chao, wakaamua kuiga sayansi kwa kumchezesha Kai Havertz kama mlinzi wa kushoto lakini wakawa wamechelewa, wakafa 3-2 kwa Uturuki.

Ujerumani inabidi wakubali kwamba kizazi cha dhahabu kimeisha, inabidi waanze chini. Kama Uingereza na Uholanzi walivyofanya.

Wakiendelea na udadisi wao watakufa kama ambavyo Italia. Wamekosa michuano miwili ya kombe la Dunia mfulululizo na juzi ilibaki kidogo washindwe kufuzu Euro

DAR NA WATU WAKE










Hawa watu wana nini, kila siku najuliza,
Mkiongea simuni, kweli watakuduwaza,
Ni mabingwa wa kughani, maneno watakujaza,
Ila jichanganye wende, utajuta kuzaliwa.

Juzi nilikuwa hapo, sema kazi za ofisi,
Atakweleza alipo, ukija kuna nafasi,
Karibu siye tupo, tena tutajinafasi,
Ile jichanganye wende, utajuta kuzaliwa.
Ataleta na matani, atakutoa ushamba,
Jiji utalitamani, kichwani utaliumba,
Jiji lisilo uduni, vile wanavyojigamba,
Ila jichanganye wende, utajuta kuzaliwa.
Mwezi ujao nakuja, utakuwa na nafasi,
Sema lini bwana waja, nipange mambo binafsi,
Tarehe utaitaja, bwana usiwe na wasi,
Ila jichanganye wende, utajuta kuzaliwa.
Kwa kuwa siyo ling'ombe, utapanga na bajeti,
Hutaki maji uombe, au undiwe kamati,
Wajipanga mkatambe, kipato chako cha kati,
Ila jichanganye wende, utajuta kuzaliwa.
Kakangu nipo mjini, nimefika tangu jana,
Ukisha toka kazini,ni vyema tukaonana,
Halafu tukae chini, sizijui nyingi kona,
Ila jichanganye wende, utajuta kuzaliwa.
E bwana huna habari, ninalo shamba Kimbiji,
Niko bize siyo siri, shamba naliweka mboji,
Vipi utanisubiri, au siyo mkaaji,
Ila jichanganye wende, utajuta kuzaliwa.
Pole sana usijali, ukija tutaonana,
Vipi Kimbiji ni mbali, cha mana jijini sina,
Tutete lile na hili, n'one mnavyopapana,
Ila jichanganye wende, utajuta kuzaliwa.
Wala usihangaike, nikupe namba ya Migi,
Popote akupeleke, kwangu kijana hazugi,
Ni kwa nini uteseke, kuja huku utabugi,
Ila jichanganye wende, utajuta kuzaliwa.
Wawaza Migi ni nani, humjui hakujui,
Heri urudi nyumbani, sije kutana na chui,
Wajipoteza hewani, kisha jijini hukai,
Dar na watu wake, usiende kichwa kichwa.

Thursday 12 January 2023

WHEN THE STORM COMES


 












 Whether it's a rain storm, 

 I will take off my coat,

 hide you like a tent, 

When the storm comes, I will protect you my love.


I will protect you, dear, 

in words and actions, 

Importantly, I will love you,

When the storm comes, it will not bother you.


It will find me strong, 

and fulfill the duty, 

The duty of a good father, 

A responsible father, 

And a wise husband,

When the storm comes, I will keep you safe. 


I will keep you safe, 

give you the victory, 

The nonsense will stop, 

When the storm comes, I will be your shield. 




I will be your shield, 

you and our children, 

I don't waver here and there, 

betrayal is not a personality, 

When the storm comes, believe that you are safe. 


Believe you are safe, 

safe heart and body, 

You will remain a mother, 

I will not stop working, 

whenever I get a deal, 

When the storm comes, it will find us strong


Monday 9 January 2023

MY LOVE

 














Beloved of my heart,

 Comfort of my soul,

 my hub a queen. 


What should I write to you, 

What is worth, 

I will never leave you.


 What gift should I give you?

 Please it's not candy,

 Although you like it, 

Your value has gone up.


Come closer dear, 

Come and start a fantasy,

Come on don't crack, 

Let me give you a job. 


Honey, I'm glad you're just for me, 

Love me without fear, 

I can't say goodbye. 


Be the stalk of the seed, 

Think of me every morning, 

With love I shall remain awake.

May we return to old age, 

Beloved, get used to me, 

Until we falter, 

Similarity is no argument. 


If I'm tired, 

kiss me, 

squash me for a joke, 

Don't afraid to laugh at me, you won't be freed. 


HIS HYPOCRITIC SONG


 

It's a catchy song, anyone with an ear,

Those who sing to him, who love his coming,

And it's a lie for them, , 

He is finished, with his own songs, 

He will make you laugh, turn around and scream, 

Always the victim.


If there is a black one, the bets crush the white one, 

If he is on the bus, let's be afraid of the plane,

Today he will crush a pumpkin, tomorrow he will praise it, 

Call the hill a park, if you want to run,

When the rain comes, he will praise the sun.


What he will praise, let us see the soothsayer, 

And pretending to be giving you a secret.

His reputation is to forget, he is a champion of ignoring, 

He does not want to lower the stake, if the truth informs him, 

We will not see scorners, claiming you are lying, 

His hypocrite song, this never stops. 



If you want to sing with him, don't raise your voice, 

Also give up your mind, let him monopolize it,

Lies to honey, others to hurt,

Let me tell you one thing, 

Do the trick, avoid him immediately, 

His hypocrite song, this never stops.

ALONE

 







Alone


My heart is lonely, my love is longing,

But I am kicked and worthless,

Where are you? Come on, don't apologize.

Since you left me,

I am crying without mercy, I do not know my wrong.


It's not an empty joke, my heart is lonely,

I do not like soup anymore, nor do I love corn.

I m not into groups, I've been lonely,

Everyone has, no one is single,

If I go astray, I may lose my back,

My path is painful, half broken my legs.


I sleep with my eyes open, waiting for the message,

The door I leave open, every day,

When I call my parents, they feel sorry for me.


Tears stop me, I write I cry,

If you are listening, come and I will take you in,

Basically consider, I love you too,

Write to me and let me know, if you see you might like.