ads

Tuesday 19 January 2016

HADITHI; REHEMA WA NJIA PANDA


MTUNZI: Moringe Mhagama
Jiunge na kundi langu la WhatsApp kwa 0717308038
KITABU CHA KWANZA

"Oyaa, madenti subirini abiria waingie’’
‘’We dogo nitakufumua hembu sogeza kongoro zako pembeni"zilikuwa ni miongoni mwa kauli zikaharishazo za makondakta kila asubuhi na mchana wanafunzi waelekeapo na watokapo shuleni.Ni wakati ambao makondakta wanakuwa na kiburi kwani wanakuwa na uhakika wa kuwapata abiria ambao wakati huo huwa wanaenda na kutoka kwenye mihangaiko ya kutafuta riziki.
Matusi na kusukumwa na hata kichaniwa sare za shule ni mambo yaliyoonekana kuzoeleka masikioni na machoni mwa watu ingawa palikuwa na wachache waliokuwa wakikereka na hali hiyo huku kauli za kejeli kutoka kwa watu wengine zikiwakatisha tamaa watu hao walikuwa wakijaribu kuwatetea wanafunzi ambao serikali iliwapa haki ya kulipa nusu ya nauli ya kawaida.
Hayo yote yalikuwa yakitokea katika kituo kidogo cha mabasi cha Njia ya Ng'ombe kilichokuwa nje kidogo ya mji wa Moshi.
Miongoni mwa wahanga wa kauli na manyanyaso hayo alikuwa Rehema Martin aliyekuwa akisoma darasa la tano katika shule ya msingi Kiwanja cha ndege karibu kabisa na kituo hicho kidogo cha magari.Ni kama vile alikuwa na damu ya kunguni kwani alionekana kuchukiwa na karibu kila konda aliyekuwa pale stendi.Hiyo yote ilitokana na tukio lake la kudai kuwa alikuwa ameibiwa nauli ndani ya gari kila alipotakiwa kutoa nauli mara tano mfululizo tena kwenye magari tofauti kitu kilichomfanya kila kondakta na hata madereva kutomruhusu kupanda garini hata kama angewaonesha nauli kitendo chake cha kusafiri bure wiki nzima kilionekana kuwachukiza hata wanafunzi wenzake ambao wakifika stendi ilikuwa ni lazima kwao kumtambulisha kwa konda kuwa huyo ndo Rehema wa Njia panda kwani wiki alilokuwa akisafiri bure kama mchezo kila walipofika eneo lililoitwa njia panda alipotakiwa kutoa nauli alidai kuwa alikuwa ameibiwa hatimaye Rehema likawa jina lake na Njia panda likawa jina la baba yake.
Baadaye ilikuwa ni vigumu kwake kupata gari la kupanda si asubuhi si mchana hata kama angekuwa na nauli na kupelekea kufikia uamuzi wa kuanza kutembea kwa miguu mara chache alibahatika kupata rifti mwenye magari mengine yasiyo ya abiria.
Kutoka kwao Rehema hadi shuleni alitumia saa moja na dakika kumi na tatu kutembea hivyo alikuwa akifika shuleni na nyumbani kwa kuchelewa tena akiwa hoi hali iliyopekea kuanza kushuka kitaaluma.
Alishawaeleza walimu wake na mama yake ambao walilipokea jambo hilo kwa namna tofauti, kwa upande wa walimu hawakulipokea kwa umakini jambo hilo, kwanza kwa kuwa Rehema hakuwa miongoni mwa watoto watu waliokuwa wakifahamika pale shuleni ama kwa mali za wazazi wao au umaarufu wao pia hakuwa miongoni mwa wanafunzi walikuwa na akili sana darasani hivyo mateso yalionekana ni haki yake kuipata.Kwa upande wa mama yake hakuwa na cha kufanya ingawa ilimuumiza sana zaidi ya kumwombea kwa Mungu wake ambaye kwake aliamini kama akimwadhibu kwa dhambi alizokuwa amezitenda ujanani ama aseme utotoni.
Alikumbuka historia yake iliyokuwa ikimuumiza siku zote huku akimwomba Mungu kumuadhibu kwa namna yoyote lakini si kwa kumfanya mwanaye apitie maisha kama yake akiwa hai ama akiwa mfu.Alijua kabisa hakumjua baba halisi wa mwanaye kutokana na matumizi ya ujana wake.
Siku zilikatika huku Rehema akizidi kuporomoka kitaaluma kutokana na mateso aliyoyapata kutembea masaa mawili na nusu kila siku ilikuwa ni zaidi ya mazoezi ya marathoni waliyokuwa wakiyafanya wanariadha kila ilipokaribia machi kila mwaka.Marafiki wachache walianza kumpa sapoti hasa nyakati za jioni ili kumpa faraja binti huyo ambaye hadi umri huo hakumfahamu kwa jina wala sura baba yake ambaye mama yake alimwambia kuwa alifariki kwa ajali mbaya ya gari iliyotokea siku mbili baada ya kuzaliwa kwake.
Alionekana ni mtu aliyekuwa na mateso makubwa sana kwa kila aliyemwangalia licha ya kulazimisha tabasamu usoni pake ,tabasamu ambalo lilikosa afya liliupoteza uzuri wa sura yake huku nywele zake ndefu nyeusi na rangi nyeupe iliyouficha weusi ulioonekana kwa mbali kwenye ngozi yake vilimfanya kila mtu amuweke kwenye kundi la watu waliochanganya damu ya kiafrika na kizungu.Lakini licha ya uchotara wake Rehema alionekana kuing'ang'ania sura ya kirembo aliyokuwa nayo mama yake Tumaini Martin ambaye kama si moshi wa kuni wakati wa kupika pombe ya kienyeji maarufu kwa jina la 'Dadii' ili kuikimu familia yake basi angekuwa miongoni mwa kumi bora ya akina mama warembo mjini Moshi.Miaka thelathini na sita aliyokuwa nayo aliiamini yeye pekee lakini kila aliyemwangalia alimwona kama binti wa miaka kumi na tisa ama ishirini na mbili.
Hakuwa na mtoto ama ndugu mwingine pale Moshi zaidi ya bintiye Rehema ambaye tangu akiwa mdogo alianza kukutana na mateso makali baada ya kuugua ugonjwa wa ajabu uliomfanya avimbe kichwa upande mmoja.
***
Tumaini Martin wengi wakipenda kumwita Tuma alikuwa mtoto wa tatu kati ya watoto watano wa mzee Martin Kasuku na Lydia Kilongo waliokuwa wafanyabiashara mkoani Dodoma.Mzee Kilongo alikuwa miongoni mwa askari wastafu wa Jeshi la Wananchi aliyekuwa na cheo kikubwa jeshini.
Alikuwa na watoto watoto wakiume wanne waliokuwa na sura za kutisha na mtoto mmoja wa kike ambaye alikuwa na sura nzuri illiyokuwa ikimvutia kila aliyeiona ama kusikia sifa zake.Wengi walimtuhumu Bi Lydia kuwa huenda alichepuka alivyoenda kuwasalimia wazazi wake huko Kyela kwani binti alikuwa mrembo haswa.Uzuri wake ulivumbuliwa tangu akiwa mdogo na kadri alivyokuwa akikua ndivyo vitu vingi vilivyokuwa vimejificha kwenye mwili wake vilijitokeza na kumfanya kila mzuri mjini pale alinganishwe kwanza na binti huyo ambaye aliiibua matumaini ya wazazi wake kupata mtoto wa kike na kupewa jina la Tumaini.
Akiwa darasa la saba Tumaini alikuwa ni miongoni mwa wanawake waliokuwa wakifuatiliwa kimapenzi na wanaume wengi mjini Dodoma.Wazee,vijana,matajiri ,masikini waliokuwa na kazi na wale wenzangu na mimi akina pangu pakavu tia mchuzi walijaribu bahati yao suala alilolifikisha kwa baba yake kupitia mama yake ambaye hakuacha kuwaadhibu vijana aliokuwa akiwakuta na binti yake.
Siku moja jioni kama ilivyokuwa kawaida yake wakiwa jikoni na mama yake Tumaini alionekana mtu mwenye wasiwasi sana hali iliyomfanya mama yake ahisi kuwa binti yake alikuwa na jambo lililomfanya awe katika hali hiyo.
"Mbona hivyo Tuma, kuna tatizo?" Aliuliza Lydia.
“Hakuna tatizo mama “alijibu Tuma huku akizuia machozi kushuka.
"Niambie mwanangu mie ni mama yako niambie jambo likusumbualo nitakusaidie"Alibembeleza mama yake.
“Hutoniamini mama"
"Niambie mwanangu nitakuamini, mangapi umeniambia nikakuamini?"
"Yote yalikuwa madogo hili hamtaliamini mama"
“Au ndo hao wanaume wa kila siku? We u mrembo lazima wakusumbue cha msingi kuyazingatia tuliyokueleza umri na wakati haujafika mwanangu" mama mtu alizidi kutoa nasaha.
“Ndiyo wanaume mama"
"Wanakutisha Leo?" 
"Hata hawanitishi, ila huyu wa leo amenitisha"
"Namfahamu?"
"Ndiyo"
"Nani"
"Baba Zita"
"Acha kuchuma dhambi binti yangu, baba Zita mchungaji? We mtoto unataka kugombanisha watu si bure"
"Ndo maaana nilise,,,,,,,"
"Kimya shetani wewe umetufanya watoto" Aliongea Bi Lydia kwa hasira akimalizia na kofi lililokwepwa kiustadi na kutua juu ya sufuria iliyotoa ukelee baada ya kufika sakafuni na kumshtua Mzee Martin aliyekuwa sebuleni na wanawe wa wawili mwisho na kuelekea jikoni.
Anord Mwakibale au Baba Zita kama wengi walivyozoea kumwita alikuwa Mchungaji wa kanisa la "The End" lililokuwa limeingia nchini miaka ya tisini huku likisifika kwa kuwa miongoni mwa makanisa machache yaliyokuwa na uwezo wa kuwaponya wagonjwa, kuwafanya vipofu waone, viziwi wakasikia na hata viwete wakatembea.
Mchungaji Mwakibale alifahamika si tuu Dodoma pekee bali hata nje ya Afrika kutokana na kazi yake kubwa ya kuokoa maelfu ya wanadamu waliokuwa na shida mbalimbali kwa miujiza na wokovu.
Urafiki wake na Mzee Martin ulianza miaka mingi iliyopita kipindi wapo shule ya sekondari ya wavulana Tabora.Walitengana kwenye mafunzo ya Jeshi La kujenga Taifa ambapo Martin alipelekwa Oljoro na Anord akipelekwa Kanembwa.Walikuja tena kukutana chuo kikuu cha Dar es salaam ambako waliurejesha urafiki wao hadi walipomaliza na Martin aliporejea jeshini kwa Mara ya pili safari hii akiingia Jeshi la wananchi na Anord akipangiwa kazi mkoani Tabora kama Afisa manunuzi wa Mkoa.
Miaka mitano baada ya kuanza kazi Anord alipatwa na ugonjwa wa ajabu.Ilikuwa Siku ya jumamosi kama kawaida yake alikuwa na mazoea ya kufanya ziara za kushitukiza kwenye ofisi zilizokuwa chini ya idara yake wilayani.Akiwa ndani ya gari la serikali ambalo lilitumika tangu zama za ukoloni Anord alimwona mtu ambaye kama aliwahi kumwona mahali.
Akamwambia dereva wake asimamishe gari, kisha alishuka na kuelekea upande aliomwona yule mwanamke.Baada ya hatua kama tatu macho yake yakakutana na mwanamke aliyekuwa akimfuata akiwa amekaa chini ya mti wa maembe.
Alijikuta akishindwa kabisa kusogea, akajaribu kunyanyua mdomo wake aseme kitu lakini mdomo wake nao ukawa mzito kutamka kitu .Wakabaki wakitazamana tuu bila kuongea chochote.
Macho yao yalijaribu kuzungumza lakini nayo yalipoteza uwezo huo, kila alipojaribu kumwongelesha kwa macho alishindwa.
Baada ya kuduwaa kwa takribani dakika mbili, hatimaye macho yao ama tuseme nafsi zao zikazungumza.
“Njoo, mwenzako nateseka hapa"
“Mie siwezi mrembo wangu, njoo wewe"
“Mie siwezi nipo kifungoni"
"Kifungoni! Kakufunga nani? "
Waliendelea kujibishana kwa hisia huku kila mmoja akionekana kumhurumia mwenzake.
“Bosi si unaliona wingu twende barabara itachafuka" Sauti ya dereva wake ilimshtua Anord ambaye ni kama alikuwa amerudishwa kwenye ulimwengu mwingine na kumfanya afikiche macho kuhakikisha kama alikuwa akiota.Hakumwona yule binti aliyekuwa akiongea naye kwa hisia bali watu wengi wakiendelea na shughuli zao za kila siku huku wakionekana kuchukua tahadhari ya mvua iliyoonekana kutarajiwa kunyesha.
“Hivi nimetumia muda mrefu sana?" Aliuliza baada ya kuingia garini.
“Umemaliza dakika thelathini ukishangaa watu" 
"Acha uongo wako wewe hata dakika tano hazijafika" 
“Tano?, we kweli umechanganyikiwa" aliongea akiondoa gari.
“Nimechanganyikiwa, mpumbavu mkubwa wewe kwa hiyo bosi wako amechanganyikiwa? Hembu nipishe hapa nimekuajiri upate kulisha familia yako nawe unajitia kidume kuniona nimechanganyikiwa, toka mpumbavu wewe" aliongea Anord kwa hasira huku uso wake ukibadilika na kuwa mwekundu.
Tangu aanze kufanya kazi kama dereva wa afisa manunuzi wa mkoa ule miaka minne iliyopita hakuwahi kumwona bosi wake akiwa amefura kiasi kile huku akisifika kwa kuwa na utani mwingi kwa wafanyakazi waliokuwa chini yake.Alimtania na kutaniwa na kila mtu bila kujali nafasi yake au jinsi, mabinti walitania na kumaanisha kuhitaji ndoa naye lakini aliishia kuwaambia ataoa Mbeya tena mke wa kutafutiwa na bibi yake.
Lakini kwa wakati ule alionekana kutokuwa Anord aliyezoeleka, dereva alitoka garini kuzuia jambo lolote baya kumfika kutoka kwa bosi yule kinyonga aliyegeuka mbogo ghafla.
Baada ya dereva wake kushuka aliusogelea usukani akiwa na hasira na kutaka kuendesha gari lakini alijikuta akilegea na kuangukia usukani jambo lilimfanya dereva wake aliyekuwa akimwangalia arudi garini na kumwangalia bosi wake ambaye licha ya kumtimua garini muda mfupi uliopita alikuwa akimwona kama ndugu yake wa damu tangu siku ya kwanza ambapo alimchukua kwa shangazi yake miaka mitano iliyopita na kupeleka chuo cha ufundi Ifunda alikojifunza Umakanika na udereva kisha kumwajiri kama dereva wake.
Aliingia garini na kujaribu kumwinua, Anord alijaribu kumzuia huku akijaribu kuzungumza kitu lakini alionekana kuishiwa nguvu kabisa hata zile ndita zilizokuwa usoni lake zilikosa nguvu na kuonesha sura iliyojaa unyonge.Alifanikiwa kumweka kwenye siti ya pembeni na kumfunga mkanda kabla ya kuwasha gari kwa kasi ya ajabu kuelekea hospitali.
Alipofanikiwa kuiweka gari lile la kizamani barabarani sawasawa hakuwaza kitu kingine zaidi ya kutaka kujaribu kuokoa maisha ya bosi wake.Akiwa katika kasi ya ajabu alishtuka kuona roli la kampuni ya tumbaku ikiwa ipo katikati ya Barabara huku watu kadhaa wakihangaika kufungua tairi la mbele, hakufanikiwa kufikiria kitu zaidi na kujikuta akijigonga kwenye kitu kizito na giza totoro lilikamata macho yake.
Mafundi waliokuwa wakitengeneza Lori walipoona gari ikija kasi mahali walipokuwa wamesimama waliamua kuyanusuru maisha yao kwa kukimbilia pembeni ambako waliamini wangekuwa salama.
Kilichofuta wengi walishindwa kukisimulia japokuwa walikuwa wamekishuhudia kwa macho yao mawili mazima bila hata kasoro yoyote.Kilichoshuhudiwa ni mwili mmoja kutolewa kupitia kioo cha mbele cha gari kabla ya kutua juu ya lori na kutua chini ambapo mapande ya nyama zenye damu yalionekana yakiwa yamesambazwa barabarani.
Gari liligonga lile lori na kutupwa pembeni na kama ilivyokuwa kawaida watu walilisogelea na kuanza kuchungulia kilichokuwemo ndani mwake.
Hakuna aliyeamini alichokishuhudia ndani ya lile gari dogo na kumfanya kila aliyeona asogee pembeni na kumtaka mwenzake aone alichokiona na kuhakikisha kama naye ataamini.
*****
Watu wote waliokuwa wamelizunguka lile gari huku wakishangaa kuona mtu ambaye alikuwa kwenye ajali mbaya kama ile kusinzia ndani ya gari na kuota ndoto ambayo bila shaka na ilikuwa ya mahaba kutokana na jinsi alivyokuwa akifanya kabla ya kujibamiza kwenye Chuma kilichokuwa kimechomoza na kumsababishia jeraha kubwa lililokuwa likitoa damu nyingi sana na kurukia nje .Walimtoa mtu yule na kumpa huduma ya kwanza kuzuia damu kutoka kisha kumpakia kwenye gari lingine lililokuwa limesima baada ya njia kuzibwa na magari yaliyokuwa yamepata ajali.
Anord licha ya kuwa na jeraha kubwa lililokuwa likimtisha kila mmoja aliyeliona hakusikia maumivu yoyote huku akikumbuka ndoto aliyokuwa akiiota.Alimkumbuka Sikujua lakini aligundua Sikujua yule alikuwa na nywele ndefu na mweusi zaidi ya Sikujua aliyekuwa akimfahamu.Lakini zaidi alikumbuka kuwa Sikujua alikuwa ameolewa huko Dodoma miaka miwili ikiyopita na ni yeye ndiye aliyempeleka stesheni ili akapande treni.
''Hapana !'' Anord alijikuta akiongea kwa sauti kubwa na kuwashtua wauguzi waliokuwa wamembeba kwenye machela kumwingiza wodini.
Baadaye aliamua kulala tena baada ya kugundua kuwa kushtuka kwake kuliifanya damu iendelee kutoka kichwani pake.Ndani ya wodi madaktari waliendelea kuhangaika kuokoa maisha yake lakini akili ya Anord ilikuwa ikimfikiria mrembo ambaye alikuwa amempa raha usingizini.Hakutaka kabisa kufanya kitu kingine zaidi ya kutaka kupata utamu ambao Sikujua wa usingizini alikuwa akiendelea kumpatia.
Masaa kadhaa ya kusafisha na kushona jeraha lililokuwa kichwani kwa Anord alijaribu kurejesha kumbukumbu kichwani mwake na kurejesha akili hiyo kwenye ulimwengu wa kawaida , alikumbuka tangu alipomwona msichana mrembo ambaye walijibishana kwa macho ,ugomvi na dereva wake na kisha kumfukuza.Akili yake ilimkumbusha pia chanzo cha ugomvi wao, ambacho alijua kabisa kuwa hakuwa sababu ya kumfukuza ndugu yake ambaye alikuwa ameenda kumchukua kijiji kwao.Hakujua kabisa kuwa ndugu yake huyo ambaye ndiye dereva wake aliyekuwa amemfukuza masaa machache yaliyopita hakuwa tena hapa duniani bali alikuwa ameshafariki.
Akili yake haikumwambia kuwa aliyekuwa akiendesha gari alikuwa si yeye bali dereva wake aliyekuwa amefariki.
Alifikiria mahali ambako ndugu yake huyo angekuwa, alijua kabisa alikuwa amemsababishia mateso bila sababu yoyote ikizingatiwa kuwa alikuwa ugenini ambako kwa haraka haraka suluhisho lingekuwa ni kushinda kwenye mashamba ya tumbaku kufanya kazi jambo ambalo hakutaka kabisa litokee.
Majira ya saba mchana gari la serikali lilifika hispitalini na kumchuka kwani alikuwa si mtu wa kulazwa huku mwenyewe akiwa hana maumivu yoyote zaidi ya kutishwa na wingi wa damu iliyokuwa imemwagika.
''Pole kwa msiba ndugu yangu'' Aliongea dereva aliyekuwa akiendesha gari walilokuwa wamepanda baada ya kumfikisha nyumbani kwake.
''Msiba nani amekufa?"
“Dereva wako mlipopata ajari alipoteza maisha pale pale''
Anord alijikuta akishindwa kujizuia taratibu machozi yalimshuka na akajikuta akikaa chini pale pale mlangoni.Hapo ndipo kumbukumbu kuwa alikosa nguvu mara tuu alipotaka kuendesha gari.Aligundua kuwa dereva wake ndiye aliyekuwa anaendesha gari pia taswira ya tukio la kuchomwa na chuma ndani ya gari ilijirudia kichwani kwake alijiona akiwa kwenye kiti cha pembeni huku nyama na damu zikiwa zimesambaa ndani na nje ya gari.Alijilaumu sana kwa kitendo chake cha kugombana na dereva wake kwani alihisi kuwa kumgombeza kulimfanya aendeshe gari huku akiwa na mawazo hatimaye alikosa umakini kabla ya kupata ajali hiyo.
Hayo yote yalipita akilini mwake haraka haraka sana akiwa palepale chini mlangoni.
Alisaidiwa kuingia ndani na yule dereva aliyemleta kabla ya kuja wafanyakazi wenzake waliokuja kuandaa mazingira ya msiba kwani marehemu alikuwa akiishi naye kabla mauti kumfika na yeye pekee ndiye aliyekuwa ndugu pale Tabora mjini ndugu wengine walikuwa Sumbawanga ,Kigoma na Dodoma wengi walikuwa Mbeya na kwa njinsi mwili wake ulivyokuwa umeharibiwa isingewezekana kuusafirisha hadi Mbeya.
Siku iliyofuata ndugu na jamaa kutoka sehemu mbalimbali walikuja kujumuika na wafanyakazi wengine kuuweka mwili ule kwenye nyumba yake ya milele.
Hakuna aliyejua kilichokuwa nyuma ya ile ajali wengi wakiamini ilikuwa ni ajali ya kawaida iliyokuwa imetokana na mwendokasi.
Siku, wiki na hatimaye miezi ilipita lakini kidonda kilichotokana na jeraha la ajali kiliendelea kuongezeka na kutoa harufu kali iliyopekelea watu kuogopa kuwa karibu ya Anord.Japokuwa mwenyewe alidai kuwa alikuwa hapati maumivu yoyote lakini wenzake walidai kichwa chake kilikuwa hatarini sana kutokana na hali yake.
Wakati hayo yakiendelea ile ndoto tamu ilikuwa ikijirudia kila siku lakini hakuna siku aliyokuwa amefanikiwa kufikia hatua ya kulila tunda.Ndoto haikuchagua sehemu ya kutokea nyumbani ndani ya gari ofisini na popote pale ilipojisikia kutokea.
Kila mara Anord alijikuta akiaibika kuchafua nguo zake kwa madafu lakini licha ya aibu ile aliifurahia ile ndoto na kutamani imtokee tena.
Sauti za kugugumia utamu ndizo zilizokuwa sababu ya wafanyakazi waliokuwa ama juu yake au chini yake kupata cha kuongea ili atoke.
" Hivi unajua Anord amekuwa kichaa?" Katibu wa Anord alikuwa aakimweleza mfanyakazi mwenzake.
''Yule atakuwa na jini asipotembea atapata shida au kufa kifo kibaya....''Alimjibu mwenzake ambaye kabla ya kumalizia jibu lake alimwona Anord ambaye alionekana amesikia kila kitu.
''Umesema nini?"Anord aliuliza akiwa amefura kwa hasira.
''Sijasema kitu mbona umefura hivi?"Alijibiwa Anord jibu ambalo halikumwingia kabisa akilini.
" Nitapiga mtu hapa si mmesema habari za wehu na majini yenu?"
"Utakuwa umesikia vibaya hatujasema habari hizo ndugu''
"Halafu we mfupi ka Kisebengo unajifanya unajua kiherehere sana'' Anord alionekana kutokuwa na mchezo hata kidogo akimsogelea mfanyakazi mwenzake aliyekuwa akipendelea kumwita Kisebengo kutoka na kimo chake kifupi.
''Jamani mbona unapenda sana kunionea jamani ''Kisebengo alimlalamikia Anord ambaye walitofautiana tuu vitengo ye akiwa mhasibu wa mkoa.
Japokuwa wote walionekana ni vijana wa rika moja Anord daima alionekana mwenye mamlaka juu ya wenzake kwanza kutokana na kuwa na muda mrefu kwenye ile ofisi huku yeye akifanya kazi zote kama mhasibu na afisa manunuzi wa mkoa wa Tabora.
''Samahani jamani lakini jiangalie Anord haya mambo si ya kawaida''Yule mfanyakazi mwingine alishauri akimtetea Kisebengo na kumpa ukweli Anord ambaye kila mtu pale ofisini alijua kuwa alikuwa kwenye matatizo makubwa.
''Na we unanitafuta kila siku ''
''Nani mimi"
''Ndiyo kila siku kazi kuwateta wenzako tuu na kuingilia hata yasokuhusu''
''Eti jamani mie kosa langu nini ?"
''Hulijui kosa lako ehhe ?"
''Ndiyo, au nilivyokushauri?''
''Umenishauri zaidi ya kuongea mambo ya kuongea wanawake?"Anord alionekana kupandwa na jazba kabisa yaani hata mtu angemwita jina lake kwa wakati ule lazima angemgeuzia kibao na kumchapa.
''He! Na wewe ukiwa na shida tusikuambie? Ngoja tuu tukuambie ukweli wewe una matatizo makubwa kama ndugu na majirani zako wanaogopa kukuambia ukweli wakisubiri mahoka wa babu zako wakuambie wanakupoteza nakuambia kwa mema kama utanichukia sawa ila hapa umeshapata hasara''Kisebengo alijitutumua na kumwambia Anord ukweli ambao hakupenda kabisa kuusikia kwani alihisi kuonewa.
Kila neno lililokuwa likitafsiriwa na akili yake lilionekana kumchoma lakini si kwa kumfanya awe mpole kwa kuwa ni la kweli bali lilikuwa likimpandisha hasira zake alijitahidi kujizuia lakini hatimaye alijikuta akirusha konde lililokwepwa kiustadi na kisebengo ambaye aliliona tangu likiandaliwa.
Anord hakukubali akatupa jiingine ambalo liliyompata Kisebengo kisawasawa kwani alionekana kuzubaa baada ya kukwepa konde la kwanza.
Kisebengo alipelekwa mlangoni alikojipigiza na kupata maumivu ambayo yalimpandisha hasira.
Aliinuka na kumparamia Anord ambaye hakujiandaa kwa kumchapa ngumi ya uso iliyompata sawasawa na kumpigiza ukutani na kutua chini kama mzigo jambo lililowafanya kisebengo na mwenzake wapate hofu na kumwinua Anord ambaye alikuwa ameshapoteza fahamu.
Pona yao walikuwa watu watatu pekee kwani wafanyakazi wengine hawakuwepo mahali pale ofisini kwa kuwa ilikuwa asubuhi sana tena Siku ya jumamosi ambayo haikuwa siku ya kazi kwa ofisi nyingi pale mkoani na hata ofisi zilizokuwa zikitoa huduma zilichelewa kufunguliwa.
Akiwa katika kupoteza fahamu Sikujua alimtokea kama ndoto zake za siku zote lakini siku ile alionekana mwenye furaha sana.
''Mbona unaonekana umefurahi sana mpenzi?" Anord aliuliza akimwangalia Sikujua kwa macho ya uchu kwani alionekana amependeza kuliko Siku nyingine alizokuwa akimwota.
''Ninakucheka wewe''
''Mimi! Nachekesha?"
“Ndiyo unahangaika kufuta damu na kitambaaa ukihisi jasho" 
''Kweli nilijua jasho kweli''Anord aligundua hilo baada ya kujiangalia mkono wake uliokuwa unelowa damu, ajabu hakusikia maumivu yoyoyote.
''Hivi nimeumia sana?"
'Ndiyo lile kovu lako la ajali limefumuka tena, lakini tuachane na hayo leo ni siku ya furaha sana maana ni siku ambayo nitakuwa na wewe wakati wote maishani mwangu''
''Kweli ?"Anord aliuliza kwa wahka.
''Kweli mpenzi wangu utaishi nami milele na utaijua sababu ya haya yote.
Anord alifurahi sana kwani alijua raha alizokuwa akiziota muda mfupi na kukatishiwa utamu njiani akuwa akizipata kila wakati.
''Au ni ule wakati ambao ulisema nitapata nafasi ya kufaidi tunda lako?".Anord aliuliza akikumbuka kuwa aliambiwa muda ukifika hawataishia njiani wala kufaidi raha usingizini bali wataishi duniani kama watu wengine wakifurahia raha lakini kwa sharti moja la Sikujua kutoonekana nje na angewambia ukweli juu ya maisha yake.
''Bado muda kufika ila ni hatua kuelekea huko''.
Licha ya kuambiwa kuwa muda ulikuwa haujafika Anord aliona ni hatua nzuri kwani hakuna kitu alichokifurahia kama kuja kupata uhuru wa kula tunda la Sikujua wa ndotoni.Alimsogelea Sikujua na kumkumbatia na kwa kuwa alikuwa amemfundishwa mambo mengi Anord alijikuta amebobea katika kumpeleka Sikujua panapohusika bila hata kutumia fimbo yake ya kurekebishia tabia.
Alimmvua gauni lake refu lililokuwa nguo pekee iliyokuwa imeufunika mwili wake na kumbeba na kumshusha kitandani kisha kumshika kiuno chake kuelekea bafuni jambo ambalo lilimshtua sana Sikujua jambo ambalo Anord hakuligundua kwani akili yake ilikuwa katika kwenda kuanzisha raha.
''Nisubiri nakuja mpenzi''Anord aliongea akirudi chumbani kupitia sebuleni jambo ambalo bila kujua lilimtisha Sikujua na ambaye kwa hasira aliinuka na kumfuata Anord na kumpiga mgongoni na kumshitua Anord aliyeshtukia yupo hospitalini huku mbele yake kukiwa na Kisebengo na yule mfanyakazi mwenzake waliyekuwa wote kwenye ugomvi.
____________
''Asante Mungu ameamka! Kisebengo na mwenzake walijikuta wakiongea kwa sauti ya juu iliyowashtua hata wagonjwa wenzake.
''Kweli Mungu mkubwa hakuwa wakupona yule''Alisikika mgonjwa alikuwa kwenye kitanda cha tatu kutoka alipokuwa amelazwa Anord.
''Maombi yamesaidia unafikiri bila kuomba angepona kweli?" Alisikika mwingine.
''Hebu nielezeni ilikuwaje?"Anord aliongea kwa kunong'oneza akimuuliza Kisebengo wakati huo akiwa amesahau kabisa ugomvi wao wa asubuhi.
''Nitakuambia ukiruhusiwa ila kiukweli haupo sawa yaani unaonekana una jini linakutesa bora tuu utembee?" Yule mfanyakazi mwingine aliongea akimkumbusha maneno ya Kisebengo ya asubuhi lakini tofuti na wakati ule Anord alionekakana kuyatafakari maneno ambayo haikuwa mara yake ya kwanza ama ya pili kuyasikia.
''Kutembea?"
''Ndiyo''
''Mhhh kwani tatizo nini?"Anord alikumbuka raha ambazo alipanga akampe Sikujua akajikuta ametopea tena kwenye ndoto yake tamu.
Anord aliporudia ndoto yake Kisebengo hakuna na kingine cha kufanya zaidi ya kumwita daktari ambaye alimkuta mgonjwa wake akiwa katika usingizi mzito hivyo aliwataka waondoke na kumwacha mgonjwa kwa madai kuwa alipewa dawa zenye nguvu sana bila kujua kuwa palikuwa na jambo nyuma ya lile jambo.
''Inawezekanaje sasa hivi niongee naye halafu alale ghafla hivi?" Kisebengo aliamua kumuuliza daktari wakati wakiwa njiani kuelekea nje ya wodi aliyokuwa amelazwa Anord.
''Inawezekana alikuwa akiongea na wewe akiwa usingizini, kwa hiyo ni jambo la kawaida tuu''Daktari alimjibu na kumwacha Kisebengo peke yake pale nje ambapo kwa mara ya kwanza alijiuliza juu ya kupata mlo kwani tangu asubuhi ya siku ile hakuweka chochote tumboni.
____
Kwa upande wa Anord alikuwa akifaidi ndoto yake maridadi ambayo daima ilimpa liwazo na tumaini akimsahau kabisa mchumba wake aliyekuwa kijijini kwao.
Aliingia chumbani ambako alichukua mkasi mdogo na kurejea bafuni ambako alimkuta Sikujua akiwa amesimama tuu kama mwenye mawazo fulani.
''Vipi mbona na mkasi mpenzi?" Sikujua aliuliza akicheka.
''Mkasi? Labda nilijisahau"Anord naye alijibu akicheka.
''Sawa urudishe basi tuoge''Aliongea Sikujua mwa sauti nyororo ambayo ilizidi mdatisha Anord ambaye alitamani kumparamia lakini alikumbuka kuwa hakutakiwa kufanya hivyo kwani ugali mbichi huumiza tumbo.
''Basi ngoja tuu kwa kuwa umefika hapa lazima utumike sogea nikuelekeze jinsi ya kushika mkasi'' Anord aliongea akimshika kiuno sikujua ambaye wakati huo hakuwa na vazi lolote mwilini.
Sikujua alimsogelea Anord karibu sana hadi kufikia hatua ya dodo zake zilizokuwa wima ziuguse mwili wa Anord ambaye alizidi kusisimka na kujikuta akitetemeka mikono yake.
''Sogea m - m mpenzii''Alibabaika Anord wakati huo alipiga magoti kwenye kistuli kulichokuwa mle bafuni na kupanua miguu ya Sikujua ambaye alijua kilichokuwa kikifuata.Kwa uangalifu na umakini mkubwa Anord alijaribu kukata nywele zilizokuwa zimeota kwa fujo kuzunguka usiri wa Sikujua.Alikata na kusisawazisha kwa vidole vyake kupima kama zilikuwa za kiwango alichokuwa akikitaka.
''Mbona una msitu hivi mpenzi?" Aliuliza Anord huku akijaribu kupitisha kidole chake kuingia ndani ambako kulionekana kupata mchocheo wa hali ya juu kwani joto na unyevu wake uliongezeka mara dufu.
''Nilikuwa nataka mwanaume wangu wa kwanza aje kuutoa" 
''Kwa hiyo hujawahi kuwa na mwanaume kabla yangu?" Anord aliuliza huku akiendelea kupunguza zile nywele kwa umakini mkubwa lakini kadri alivyokuwa akishika zile nywele ndivyo Sikujua alivyoanza kupumua kwa shida kuonesha kuwa alikuwa katika wakati mgumu.
''Ndiyo mpenzi wewe ndiye wa kwanza kwangu''
''Kweli?"
''Na wewe maswali yako hadi unaniudhi nikwambie mara ngapi? Mhhhh“Sikujua aliongea akimpiga piga Anord mgongoni.
''Siamini mpenzi natamani hiyo siku ifike haraka nifaidi hii tamu''Anord aliongea akipigapiga kichwa cha chini cha Sikujua na kunyanyua vinywele kwa vidole vyake kwa mtindo wa kuvikusanya.
''Ashhhh mhhh enheee hivyo hivyo ''Sikujua alijikuta akijipinda pinda na akajikuta akilala kwenye sinki lililokuwa na maji ya baridi huku akimpa nafasi Anord kumuosha maeneo aliyokuwa akiyafanyia usafi na maeneo ya jirani.
Baada ya kuhakikisha kuwa alikuwa amemsafisha vilivyo alimwinua na kumbeba kisha kumpeleka kitandani ambako alimfuta maji kabla ya kuchukua kopo la asali ambayo aliimiminia kiganjani na kumsogelea Sikujua ambaye hadi wakati huo alikuwa ameshazidiwa akajikuta akipeleka mkono wake mmoja usirini ambako aliuacha ukivijari huko huko huku kidole kingine kikiwa kikilambwa na ulimi wake.
Anord aliutoa mkono uliokuwa sirini na kuupa pipi kijiti ambazo kwa kipindi kile hazikuhitajika senti nyingi kuweza kuzipata na ili kuzinunua ilikuwa ni kwa ajili ya watoto.Sikujua aliipokea ile pipi na kuitoa gandani ambapo alijikuta akigeuzwa kwa mkono mmoja wenye nguvu wa Anord kisha asali kuwekwa kwa vikundi kuzunguka kiuno chake upande wa mgongoni kabla ya kuhisi kitu  chenye joto kikivinjari maeneo ya kiuno chake na kuhisi vitu vikitembea tembea mwilini mwake huku usiri wake ukizidi kuzalisha ubichi.
Baada ya ulimi kumaliza kuilamba asali iliyokuwa imepakwa mgongoni, asali nyingine nikapakwa mapajani sehemu ya nyuma ya magoti kisha zoezi la kulambwa likiendelea na kumweka Sikujua kwenye wakati mgumu zaidi kwani kasi ya kuilamba pipi kijiti ilipungua kadiri muda ulivyosogea huku sauti za kuhema zikipanda na kushuka jambo ambalo licha ya kumfanya Anord atoe ute ute kwenye silaha yake ambayo kama ingeguswa tuu basi risasi zote zingetoka kwa kasi hakushtuka wala kuacha alichokuwa akikifanya zaidi ya kuhama tuu maeneo ambapo kwa wakati huo alihamia miguuni ambapo alipaka miguu yote asali hadi unyayoni ambapo alianza kuilamba taratibu lakini hata kabla hajaimaliza asali ya mguu mmoja Sikujua alijipinda na kuacha pipi kijiti ya mzungu na kuanza kuila ile iliyotengenezwa na Muumba ambapo nayo ni kama ilikuwa imetegeshwa ilirusha risasi zilizotua kinywani mwake na kumfanya Anord ajipinde kwa raha na kuahirisha zoezi lake na kwa kuwa walikuwa wamelala kwa kupishana kichwa miguu miguu kichwa Sikujua alilamba pipi ile kwa utaratibu kuku vidole vyake vikizunguka shina la ile pipi na kumweka kwenye wakati mgumu zaidi Anord ambaye naye alijikakamua kuanza kunyonya usiti wa Sikujua ambaye ni kama alikuwa akipigwa na shoti ya umeme kwani alijipindapinda na kumgeuza Anord na kuielekeza ile pipi sirini kwake.
Kama ilivyokuwa kwa Sikujua kwa upande wa Anord naye hali ilikuwa hivyo kwani hakuwa na kipingamizi kwani aliruhusu pipi yake iingie shimoni ambako ilipokelewa kwa kiuno kilichozungushwa kwa umaridadi sana.Ilikuwa ni kama mashindano kwani kila Anord alivyoenda chini Sikujua naye alikuwa akija juu akienda juu basi atamfuata huko huko kulia alienda kushoto ili kuongeza msuguano ambao ulikuwa ndio chachu ya utamu wa zoezi.
Dakika arobaini zilipokuwa zikisha ndipo wote walikuwa wakishuka mlima mrefu ambao walikuwa wameupanda tena wakiwa wakikimbia mtu wa kwanza kushtuka alikuwa Sikujua ambaye ni kama alikuwa akirejewa na fahamu na kujishika siri  yake ambayo haikutamanika kwa kulowanishwa na dafu lililokuwa nimepasuliwa na kumwagiwa maeneo hayo.
''Paah!'' kibao kilichotua kwenye shavu la kushoto la Anord na kumzindua kutoka kwenye umbumbumbu  uliotokana na shughuli aliyotoka kuifanya.
''Mbona unanipiga Siku kulikoni?" Alilalama Anord akijipapasa shavu lake lililokuwa limepigwa.
''Umefanya nini mpumbavu wewe?"
''Nimefanya nini ama tumefanya nini?" Aliuliza Anord akicheka.
''Mpumbavu mkubwa wewe umeona nakuchekesha hapa'' Hapo kofi la uso lilitua usoni likifunika jicho lote na kuumsababishia Anord atoe ukelele wa maumivu.
''Mamaaaa nakufa!"Sauti ilimtoka Anord na kuwashtua wagonjwa na Kisebengo ambaye alikuwa ameanza kusinzia kutokana na ukimya wa mgonjwa wake.
''Nini tena Anord?" Aliuliza kwa wahka Kisebengo huku akijutia kitendo cha kujiingiza kwenye matatizo ya Anord ambaye alijua kabisa kuwa palikuwa na kitu kilichokuwa kikiendesha suala lile.
''Nimepigwa kofi la uso ''
''Na nani wewe umepigwa wapi?"
''Jicho la kushoto halafu limevimba'' Alijieleza Anord wakati huo wagonjwa kadhaa walikuwa karibu na kitanda cha Anord wakishangaa maneno aliyokuwa akiongea kwani kuna waliokuwa wakimshuhudia anavyojipiga kwenye pembe ya kitanda cha chuma alichokuwa amelalia.
''Mzee si umejigonga kitandani mara mbili, mara ya kwanza shavuni na mara ya pili kwenye jicho lako la kushoto sasa hilo kofi la kukutoa nundu umepigwa saa ngapi?" Aliuliza kijana mmoja aliyekuwa amelala pembeni yake akimwangalia Anord tangu alivyoanza kuhangaika kujigeuza huku na kule saa nyingine akilamba hewa na shuka lake.
''Kweli ona hata nywele zimebakia hapa" aliongea mgonjwa mwingine ambaye alikuwa kwenye kiti cha matairi.
'' Anaweza akawa na jini huyu si bure'' Alichangia mada mmoja aliyekuwa kwenye kundi la wagonjwa wagonjwa waliokuwa wamesimama kukizunguka kitanda cha Anord.
''Hapana huenda ni maralia imepanda kichwani''aliongeza mwingine.
Baadaye alikuja daktari kumpa dawa za maralia kama vipimo vilivyoonesha awali huku akishtushwa na uvimbe uliokuwa jichoni ambao ulionekana kuongezeka kadri muda ulivyozidi kupita .Baadaye Anord alijikuta usingizini lakini tofauti na mara nyingine usingizi ule ulimtisha na kuanza kupiga kelele ambazo zilimwamsha mwenyewe huku akionekana kama mgonjwa wa akili lakini kwa vipimo vya daktari vilionesha kuwa alikuwa na maralia kali ambayo kama walivyodai ilikuwa imekimbilia kichwani.
Hali ilikuwa hivyo kila alipopata usingizi na baada alianza kukimbia na kama si madaktari na wagonjwa wachache waliokuwa na nguvu basi Anord angepotelea mitaani huko huku akipiga kelele zilizokosa maana yoyote kwa kila aliyezisikia.
Madaktari walichukua uamzi wa kumfunga kamba lakini kila alipopata usingizi alijikuta akipiga kelele huku akitaka kukimbia jambo lililokuwa kero kwa wangonjwa wengine hatimaye akahamishwa chumba na kupelekwa kwenye chumba cha upasuaji mdogo na sindano kulikokuwa na kitanda kimoja ili afungiwe huko hadi asubuhi kwani muda huo ilikuwa saa mbili na nusu usiku.
Usiku mzima kelele zilitoka kwenye chumba alimokuwa amelalala Anord na siku iliyofuata asubuhi ulitawala ukimya kitu kilichowaaminisha kuwa alikuwa amelala usingizi mzito.
Nesi wa zamu akiwa ametanguzana na daktari waliusogelea mlango wa kile chumba ili wampeleke chumba kingine na kile chumba kitumike kwa ajili ya sindano na oparesheni ndogo.Walipofungua mlango walipogwa na butwaa kwani walichokishuhudia hawakuwa wamekitarajia.
Daktari na muuguzi wa zamu hawakuona walichokitegemea zaidi ya kitanda kilichokuwa kimebinuliwa juu chini.Kwa haraka wakainua kitanda kuona kama palikuwa na mtu pale chini lakini napo hawakuona chochote zaidi ya mashuka yaliyokuwa yamechafuliwa na matapishi kuonesha kuwa aliyekuwa amelala juu ya kile kitanda alikuwa ametapika sana kutokana na uchafu uliokuwa umechafua zile shuka.
Uchunguzi wa kile chumba ulithibitisha kuwa hakukuwa na mtu yeyote zaidi yao.
''Huyu mtu kweli alilala humu ndani?" aliuliza yule daktari akiwa haamini kabisa alichokioba kwani jana yake alimwacha yule mgonjwa mle ndani baada ya kusumbua wagonjwa wengine katika wodi.
Yule muuguzi wa zamu hakuwa na jibu lolote kwani hakuwepo wakati yule mgonjwa akipelekwa kule lakini alipewa tuu maelezo wakati akiingia zamu.Japokuwa alikuwa akimfahamu Anord lakini hakujua hadi analetwa pale alikuwa na hali gani.
''Si tumekuta mlango umefungwa?" aliuliza yule daktari akiwa bado haamini kilichokuwa kimetokea.
''Ndiyo huenda akawa ametoroshwa na ndugu zake na kukimbilia kwa waganga wa jadi.
''Kama kutoroshwa basi mlango ungevunjwa mbona mlango upo salama na tumekuta umefungwa?" 
''Huenda waliomtorosha walikuwa na funguo''
''Acha mawazo ya kipumbavu nani ana funguo za huu mlango zaidi yangu?" Alifoka yule daktari na kuanza kuondoka kwani alijua yule muuguzi alikuwa akianza kumwingiza kwenye uhusika wa tukio lile kwani ndiye aliyekuwa mtu wa mwisho kutoka mle chumbani na ndiye pekee aliyekuwa na funguo za mlango wa kile chumba.
Lakini wazo la kusema alikuwa ametoroshwa na ndugu zake lilipuuzwa na ukweli kuwa Anord hakuwa na ndugu pale Tabora zaidi ya Mbeya hivyo uwezekano wa kutoroshwa na ndugu ulikuwa mdogo sana.
Taarifa za Anord kutoweka kiajabu chumbani alikokuwa amefungiwa kupunguza kero kwa wagonjwa wenzake zilienea kama moto wa kiangazi kwenye pori zee na kusababisha minong'ono miongoni mwa kila aliyelisikia jambo hilo ,kuna walioamini kuwa alitoroshwa kwa ushirikiano wa mmoja wa wauguzi waliokuwa zamu, kuna waliokuwa wakiamini kuwa Anord hakuwekwa humo usiku uliopita na kuna wale waliona tukio lile lilihusisha nguvu za kiimani zaidi huku wakihusisha matukio ya mgonjwa huyo wakati alipokuwa akilalamika kupigwa kofi wakati alikuwa amejipigiza kitandani.
''Nilikuambia yule kijana ana jini''Alinong'ona mmoja wa wagonjwa akimwambia mwenzake ambaye alionekana kukubaliana naye kwa kulitafakari jambo hilo na kuuliza swali ambalo lilikuwa ni kama la kukazia alichokuwa ameambiwa.
''Kwa hiyo anaweza akawa ametoroshwa na hilo jini?" 
''Ndiyo , huenda ikawa hivyo maana wanadai mlango ulikutwa kama ulivyokuwa umeachwa''
''Labda ''Hao waliishia kuwaza hilo .
Daktari aliyetoa wazo la kumfungia Anord peke yake na kuondoka na funguo aliona kabisa jambo lile likimwelemea hasa baada ya askari kadhaa kuanza kuwahoji maswali kadhaa kuhusu tukio hilo la aina yake lililoharibu kabisa ratiba nzima ya siku ile.
''Una uhakika funguo za mlango ule unazo wewe pekee?" lilikuwa ni swali lililomuumiza yule daktari kwani licha ya kudai alikiwa nazo peke yake lilikuwa ni uongo ambao yeye na mtu mmoja ambaye alitamani kutaka kujua kama alienda mahali pale.
Lile swali lilizidi kumuumiza kila dakika licha ya askari polisi kuondoka pale na kuamuahidi kurudi muda wowote ama kumwita pale watakapomhitaji .
''Kwa nini alirudia sana lile swali atakuwa anajua nini?" yule daktari alijikuta akiongea peke yake badala ya kufikiri kama alivyotaka kufanya jambo lililomfanya ageuke huku na huko kujua kama kulikuwa na kiumbe yeyote aliyemsikia.
Hakuwako.

0 comments:

Post a Comment