ads

Monday 25 May 2015

AUGUST LANDMESSER,MWANAUME AMBAYE HAKUMPA HESHIMA HITLER


Na. Moringe Jonasy kwa msaada wa mtandao.
Umewahi kumsikia kiongozi mmoja wa Kijerumani amabaye alikuwa sababau kubwa ya kutokea kwa vita kuu ya dunia?
Umewahi kusikia kuhusu mateso waliyowapata Waisraeli zaidi ya milioni mbili kabla ya kuuawa ambayo yaliongozwa na Kiongozi huyo wa Kijerumani?
Kwa kusikia tuu simulizi za kukatwa viungo vya mwili ili madaktari wakijerumani wapate mafunzo kwa vitendo ama wakiwekwa kwenye vyumba vya mateso hujawahi kusisimkwa na damu yako ikapata ubaridi licha ya mambo hayo kutukia mambo mingi yaliyopita?
Najua hata akitokea Hitler ama  mzimu wake lazima utamwogopa na kumpa heshima ikibidi kwa kuogopa kukutwa na yaliyowapata Waisraheri wa miaka ile lakini kuna mwanaume mmoja ambaye tarehe na mwezi kama wa jana mwaka 1910 alizaliwa kabla ya kukua na kuishi katika zama ambazo alilazimika kuyashuhudia mateso ya utawala wa Kiongozi  huyo aliwahi kutompigia saluti.

Hiyo ilikuwa tarehe 13 juni mwaka 1936 katika gwaride la uzinduzi wa jeshi la wanamaji la Horst Wessel.
 August Landmesser(aliyezungushiwa duara) akionekana hana habari na saluti kwa Hitler(hayupo pichani).

KUMBE ALIJIUNGA NA CHAMA ILI APATE KAZI
Unawez akuwalaumu watu ambao hujiunga na vyama Fulani ili wapate kazi , basi uanatakiwa kumlaumu na huyu bwana ambaye alijiunga na NAZI kwa matarajio ya kupata kazi kabla ya kufukuzwa kwenye chama baada ya kutaka kumuoa mwanamke aliyekuwa na asili ya Israeri, Irma Eckler ambaye licha ya apta vikwazo vingi wallifanikiwa kuzaa naye watoto wawili Ingrid na Irene ambaye mkewe alijifungua akiwa kizuizini.

Mkewe akiwa na watoto wake Ingrid na Irene


ALIWAHI KUJARIBU KUKIMBILIA DENMARK
Mwaka mmoja baada ya kufukuzwa kwenye chama cha NAZI (mwaka 1937) August alijaribu kutorokea Denmark katika harakati za kulinda penzi lake lakini walikamatwa yeye na mpenzi wake kabla ya kufanikissha azma yao.
Kwa kifupi maisha ya mwanaume huyu ambaye alikuwa mtoto wa pekee kwenye familia yake yalitawaliwa na mikasa na matukio mengi ya kustaajabisha hadi pale alipopoteza maisha akiwa vitani huko Koratia Oktoba 17 , mwaka 1944 mkewe alifariki miaka mitano baadaye huku wanae wakichukuliwa na kulelewa kwenye kituo cha yatima huku wakigawana majina ya wazazi wao.

 Akiwa kwenye sare.

0 comments:

Post a Comment