ads

Monday 18 May 2015

SIMULIZI;BARUA YA BHOKE




MWANDISHI;MORINGE MHAGAMA

MSIMULIAJI;GODWIN

Miale ya jua ilimulika ikipiga mapaa kutokea upande wa magharibi kuashiria machweo yalikuwa yakichukua nafasi weakati huo.Sauti za watoto wakicheza nje ya nyumba zao ziliongeza uhai wa eneo lile, mbuzi nao walikuwa wakirudishwa mabandani mwao na wamiliki ama vibarua waliokuwa wameletw akuishi pale kwa ajili ya kazi hiyo.

Nyasi za kijani kibichi pamoja na majani ya kiti mirefu ya kupandwa yalikuwa yakipelekeshwa na upepo huku na kule kadiri ulivyotaka .

Sauti za matairi ya magari yaliyokuwa yakisugua barabara ya lami zilisikika kutoka mbali huku sauti zikerazo za pikipiki zikisikika kama vile zikishindana na na sauti za ngurumo za magari makubwa.Honi za pikipiki na taksi zilisikika si kutaka kupishwa bali kusaka abiria ambao wengi walikuwa wakitoka kazini na wachache walikuwa wakiiingia kazini.
Kina mama na mabinti zao walisikika wakipepeta mchele na kuagizana vibandani kununua viungo ambavyo ama havikununuliwa ama havikutosha , huku akina baba nao wakiwa na vijana wao wa kiume wakimwagilia bustani na kuchuma mboga za majani ambazo walipenda kudai kuwa walikuwa wakizipalilia kw akupunguza majani yaliyokuwa yamezidi.
Wakati hayo yakiendelea, ndani ya nyumba moja kuna kijana alikuwa amekaa tuu akisikiliza muziki ambao hata baada ya umeme kukata na redio kuzima aliusikia ule muziki huku akiimba kwa kumung’unya maneno ambayo hakuyakumbuka. Mwalimu Godwin Joseph alikuwa akiendelea kuimba nyimbo za msanii wa Bongo Fleva Sam wa ukweli ambazo alikuwa akizisikiliza kabla ya umeme kukata bila kujua kuwa kulikuwa na mtu aliyekuwa akigonga mlango wa nyumba yake kwa muda mrefu hadi aipochukua uamzi wa kuingia pale ndani.
‘’Shikamoo mwalimu’’Alisalimia Kurwa mwanafunzi wake shuleni Njombe sekondari ambaye kwa kipindi hicho alikuwa likizo.
‘’ Mhh-m-maa-Marhhabaa vipi umegonga sana?’’Alibabaika Godwin akisugua macho yake yalikuwa makubwa kama ma apple ya Uwemba kwa viganja vyake vilivyonyimwa nyama za kutosha kushikilia viunzi .
‘’Ndiyo mwalimu Sikai sana kuna barua yako amenipa mkuu amesema ilitumwa kwa anuani ya shule’’Aliongea Kurwa akimpa barua iliyokuwa imewekwa kwenya bahasha iliyovutia kwa rangi na urembo wake.
‘’Asante sana karibu Soda ipo kwenye jokofu fungua hapo jihudumie’’Aliongea Godwin akielekeza kidole kwenye jokofu lililokuwa limejee pombe nyingi ingawa hakuwa mnywaji wa pombe alipenda sana kuwawekea rafiki zake ambao wengi walikuwa wakipenda kunywa pombe.Alikuwa amejaribu kunywa pombe zaidi ya mara nne lakini aliishia kutapika na kupata homa hivyo akaamua kuachana nayo zadi ya kuzitazama kwenye ndani ya jokofu lake.
‘’Asante mwalimu kuna mtu nilikuwa na miadi naye namuwahi’’Alijibu Kurwa akifungua mlango na kutaka kutoka.
‘’Vipi shem nini? Maana watoto wa uzunguni ukiwakosa wakiwa na nafasi basi utasubiri mwaka tena unakuja kumwona na mshikaji mwingine wahi bhana’’Aliongea Mwalimu Godwin akicheka.
‘’Hapana mwalimu , baadaye nitakuja tuongee’’Kurwa akiongea akiwa nje ya ile nyumba.Alimzoea mwalimu wake wa Geography ambaye alikuwa ni kama rafiki yake tuu lakini alikuwa akimficha sana juu ya masuala ya mahusiano kwani licha ya mwalimu wake kupenda sana nyimbo na tamthilia za mapenzi hakuwahi kumwona akiwa na mpenzi wala kusikia akimwongelea, alijua labda kwa kuwa aikuwa akimwona kama mwanafunzi hivyo aliamua kumficha.Kauli ya kumwambia kuhusu wasichana wa uzunguni ni kweli wana tabia kama zile , je miezi tisa aliyokaa Njombe ilitosha kuzijua tabia zao bila kujihusisha nao?. Hayo ni baadhi ya mambo aliyokuwa ametoka nayo Kurwa kwa mwalimu wake ‘’msela’’ kama alivyokuwa akiiitwa na wanafunzi wake bila kujua.
Mwalimu Godwin alijikuta akipata kigugumizi kuifungua ile barua ambayo kwa mwonekano wake ilikuwa ikionesha kabisa ni suala la mapenzi lilikuwa ndani mwake lakini ni nani ambaye alikuwa ameiandika, kwa nini atumie anuani ya shule?, kwa nini aandike barua badala ya kumpigia simu? Hakuifungua ile bahasha nzuri ambayo kuifungua tuu kungekuwa kama kuharibu nakshi zake zaidi ya kuigeuza geuza pengie jina la mwandishi wa barua lingeandikwa nyuma ya ile barua lakini hakuona chochote zaidi ya nakshi za’ I Love You’ zilizokuwa na maua ya kuchorwa na kubandikwa.
Mra simu yake ilionesha kuwa palikuwa na ujumbe uliokuwa umeingia akawahi kama kibaka akikwapua mkoba wa ‘ Sister Duu’ na kufungua ujumbe ambao akili mwake alijua utakuwa umetoka kwa mtu ambaye ana wiki mbili hapatikani simuni alitamani kupata ujumbe wake.Alitamani kusikia kilichomfanya asipatikane , alikumbuka kuwa mara ya mwisho kuongea naye walibishana juu ya jambo fulani na simu ilipokatwa na huyo mtu haikupatikana tena.
‘’NDUGU MTEJA KIFUSHI CHAKO CHA CHEKA KIMEKWISHA, SASA UNAWEZA KUONGEA BURE BAADA YA DAKIKA TATU ZA KWANZA, asANTE KWA KUTUMIA VODACOM’’
Ulisomeka ule ujumbe na kumfanya asonye kwa sauti , hakutegemea kukutana na ujumbe ule aliouita wa kipumbavu kwani kila muda ule ulikuwa ukiingia simuni mwake na alijiunga tena na huduma ile kwa matarajio ya kumpata mtu ambaye wiki ya pili alikuwa akimtafuta simuni bila mafanikio.
Akiwa na na hasira juu ya ule ujumbe simu ujumbe mwingine uliiingia na haraka haraka akaufungua na kukutana na kitu ambacho pia kilimkera.
‘’NMB INAKUKUMBUSHA KUHAKIKISHA TAARIFA ZAKO ZA BENKI KABLA YA MWAKA KUISHA KUEPUKA USUMBUFU WA KUFUNGIWA AKAUNTI YAKO’’ TUNAKUTAKIA SIKUKUU NJEMA YA X-MASS NA MWAKAMPYA’’
Baada ya kuusoma ujumbe huu wa pili ulimkera ukampa mwanga fulani juu ya ile barua aliyokuwa ameipokea alijua lazima itakuwa ni kadi kwa ajili ya kumtakia sikuu njema , lakini hakuweza kutabiri aliyekuwa amemtumia kadi hiyo.
Aliifungua ile bahasha kwa umakini mkubwa, lakini ujumbe mwingine uliingia simuni , huku akisonya sonya alifungua tena ujumbe ule huku akitegemea kitu ambacho kisingemkera lakini baada ya kusoma alijikuta akiongea mwenyewe.
‘’Haya mameseji yao ya kudownload yananiboa’’alifuta ule ujumbe bila hata ya kumaliza kusoma , ulikuwa ukihusu kuisha kwa mwaka na kuanza kwa mwaka mwingine.
Akairudia tena bahasha na kuifungua yote ambapo aikutana na picha ya mtu aliyekuwa akiisubiri simu na meseji yake kwa takribani wiki mbili na barua ambayo aliifungua kwa pupa kama mtoto afunguavyo zawadi iliyofungwa kwenye boksi. CHUO KIKUU CHA MWENGE
S.L,P 2676,
MOSHI.
17/012/2014



Mpedwa Godwin
Salamu nyingi zikufikie hapo ulipo ,najua u mgonjwa kwa kunikosa hewani kwa zaidi ya wiki moja ila kwa upande wangu bado si mzima tangu uliponiachia homa yako kali ya Upendo.
Matilaba ya barua yangu ni kutaka kukuambia mambo machache ambayo naamini unatakiwa kuyajua hasa katika kipindi hiki kigumu ulichonacho.
God unajua jinsi gani nakupenda na unavyonipenda hata kabla hatujaambiana habari za mapenzi lakini pia najua hujui kuwa kuna mtu ambaye nampenda zaidi yako tana mbaya zaidi huyo mtu tumefahamina miaka miwili baada ya penzi letu.
Naamini nawe unamjua kwani mara nyingi umekuwa ukinikataza kujihusisha naye japokuwa mara nyingi nimekuwa nikikwambia kuwa pendo langu kwake halitaharibu mahusiano yetu lakini umekuwa kaidi na kuniambia kuwa nikitaka kumpenda basi nisiwe nawe kwani sikusikilizi kisa huyo mtu kitu ambacho nikuambie tuu ukweli kuwa SIWEZI KUACHA KUMPENDA.Niampenda na nitampenda japo nawe nakupenda sana .
Pengine unaweza ukawa unaisoma barua hii kwa kuacha na kuendelea kwa hasira , kwani nakufahamu God wangu nikupendaye mwanaume wangu wa kwanza na wa mwisho lakini kwa hali hii naamini hutokuwa wa mwisho.Nikupendaje we mwanaume? Nimekataa vingapi kwa ajili yako we mwanaume? Mara ngapi nimeishi kwa mashaka baada ya kuwakataa wenye mamlaka na pesa zao kwa ajili yako? Kwa nini unapenda kunitukana na kunilaumu kwa kukataa kukubaliana nawe juu ya kuwa na huyu mtu nimpendaye siku zote UANDISHI WA HADITHI FACEBOOK NA POPOTE PALE ndiye mtu nimpendaye pengine zaidi yako lakini sijui wivu , chuki na lawama zako juu ya suala hili limekufanya unitishie ama uniache zaidi ya mara tano kwa sababu ya huyu mtu.
Pengine unaamini nikiwa maarufu kwa kuandika hadithi nitafuatiiwa na wengi, lakini ujue nimefuatiliwa na wengi sana hata kabla sijaanza kuandika hadithi na nikabaki nawe. Au sijakuelewa huenda ni sababu yako ya kutaka kuniacha na kuwa na mwingine umpendaye zaidi yangu?. Sawa nitabaki na Huyu nimpendaye kwani kila uniumizapo amekuwa akiniliwaza na kujikuta nasamehe bila masharti yoyote lakini unamwona ni adui wa penzi letu.
Mwisho nikuambie nimeamua kuwa naye huyu na sitokuwa nawe hata uje na mtazamo upi kwani umeniumiza sana maksudi kwa kigezo cha kuwa sikupendi kwa sababu sikusikilizi , je wewe usiyetaka kunisikiliza unanipenda, Au imeandikwa asikilizwe mmoja tuu?.
We si yule ambaye ulijafanya uko bize na kazi ya kufundisha wakati facebook upo bize ukipeana miadi na wasichana wako wengine na mkibadilisha namba na wasichana hao miongoni mwa namba unayowasiliana nayo sana ni yangu nimetumia jina la Bitric Jochim, umeshtuka ehee we si ulisema bado humjui msichana mimi Bhoke Binti Joshua hukunivua nguo zangu? Sawa baba endeleza ujogoo wako tukuzike na kilo mbili.
Siongei sana baba nikutakie sikuu njema ya krismass na mwaka mpya 2015 ila usisahau kunitumia zawadi ulosema unanitumia kwa jina la Bitric.
Aliyekupenda……..
Bhoke Joshua Masatu…
Godwin aliirudia ile barua akiruka ruka maneno na kujikuta akilia alishindwa pa kuanzia juu ya jambo lile ambalo aliona ni gumu kuliko mambo yote aliyowahi kukutana nayo.
JE WEWE UNGEMSHAURI NINI?

0 comments:

Post a Comment