ads

Sunday 15 May 2016

NIMEYAONA HAYA BAADA YA KUSIKILIZA MOYO MASHINE


Na.Mwanakalamu
Juzi wakati nikizurura kwenye kurasa za wanamuziki nchini nikajikuta nikiangukia twitier kwenye ukurasa wa mwanamuziki  Ben Paul, hapo nikaziona post zake zikiwa na hashtag ya moyo kazi yake nini.Hapo nikajikuta nitafakari sababu ya hashtag hiyo nikaisearch lakini nikakuta ni yeye ndiye aliyeileta. Akili yangu ikafanya kazi haraka.
Wimbo mpya.
Naam sikukosea kwani dakika chache baadaye  nikasikia akihojiwa redioni nini maana ya hashtag hiyo, jibu lake likawa ni wimbo mpya kama nilivyodhani.Nikaanza kuhisi ulikuwa ni wimbo aliudharau kwa kuamua kuwashtukiza mashabiki na wapenzi wa muziki.Huenda ni bunos track isiyo na madhara makubwa, nikahitimisha na kuendelea na harakati zangu za kusaka umbea.Ndiyo kusaka umbea kama nisipoujua umbea nitaandika nini mwanakalamu maana mie umbea wako  unaokuaibisha kwangu ni naugeuza fursa na darasa wakati mwingine ni fimbo ya kuwanyoosha wasiokuwa wastaarabu.
Usiku nilikuta link ikisambaa kila mtu akiusifia wimbo wa mkali huyo wa Rnb , nikaupakua huo wimbo na kuusikiliza.Neno la kwanza kunitoka lilikuwa ni kwamba huu wimbo angeimba na Baraka Da Prince neno la pili lilikuwa ni kuwa kama nasikia ile radha iliyopotea ya Kid bway  nikaamua kufuatilia mtayarishaji , sikukosea alikuwa ni Lolly Pop yule yule mwimbaji wa Injiri na mtunzi wa nyimbo kali za bongofleva na mpishi ama muuandaaji wa nyimbo halisi za bongofleva.Nyimbo ambazo ukizisikia popote utajua ni za kutoka Tanzania nchi ya bara na visiwa kadhaa.
Hapo nikagundua mambo yafuatayo;
Ben Paul ni mwanamuziki si msanii
Ukiangalia video yake unaweza kuhisi huyu jamaa hana swag kama wenzake katika bongofleva wafanyavyo maana hakuna gorofa wala vinguo vya kuweka maungo ya wanawake nje.Lakini licha ya huko kukosa kwake swaga Ben Paul hajaweka usanii sana kwenye kazi yake bali uanamuziki unaonekana na hata wimbo wenyewe una nguvu ya kukaa kwenye charti miazi zaidi ya mitatu bila hata ya kuwa na video kama ilivyokuwa Sophia.Ben kauonesha uanamuziki wake katika kujua kupanda na kushuka kwa sauti zake huku melody za wimbo zikibeba nini mashairi yanataka.

Lolly Pop ni mkuu asiye na makuu
Kwa mara ya kwanza nilianza kujua utunzi wake pale niliposikiliza kwenye Basi nenda, wimbo ambao pia aliuandaa lakini sikuzikia akijitapa kwenye vyombo vya habari kuwa yeye ni zaidi ya Mo Music kama watunzi wengi wanavyozuka baada ya wimbo wao walioutunga ukiwa mkubwa.Nilikuwa  namsikiliza wakati anhojiwa na Saida Mwilima , kwa upole bila makuu alikuwa akiutambua na kuuheshimu uwezo wa waimbaji anaowaandikia nyimbo.Hata aliandika nyimbo za Baraka Da Prince hakuonekana kuutamani umaarufu ambao Baraka angeupata baada ya ngoma hizo kuwa kubwa bali alibaki mkimya na mwenye kuchagua maneno ya kusema pale alipohojiwa huku akijivunia kuwa mwandishi wa nyimbo za wanamuziki wenye vipaji.
Ni busara ilioje.
Lolly pop ambaye jina lake la kwenye vitambulisho ni Godluck mwimbaji wa nyimbo kadhaa za injiri ukiwemo ule wa ‘’Acha waambiane’’  bado hajaonesha tama ya kuwa maarufu huenda angekuwa mwingine angeamua kuachana na kuimba nyimbo za injili na kuhamia kwenye bongofleva anabaki kuwa mkuu asiye na makuu.
Kuna kipindi niliwahi kusoma mahali kuwa alikuwa tayari kumwandikia Alikiba wimbo buree kabisa.

Kidy Bway ni mkali wa kachumbali na melody kali

Kwa sasa ni mmoja wa wafanyakazi wa kituo kipya cha redio ya jijini Mwanza  Lake fm , kabla ya hapo alikuwa Sahara Media kabla ya kwenda Bongo five.Pia ni mtayarishaji wa muziki katika studio ya Tetemesha Record aliwahi pia kuwasimamia wanamuziki Sagna,Csir madini na Baraka Da Prince kwa nyakati tofauti pia ni moja kati ya watu ambao walichangia mafanikio ya kimuziki ya Hussein Machozi.
Kidy ni mkali wa kuweka kachumbali kwenye nyimbo zinazopitia mikononi mwake kama huamini tafuta nyimbo zote zilizopita tetemesha records pia licha ya ukali wa kutia kachumbali kwenye nyimbo hizo Kidy ambaye jina lake la kitambulisho ni Sandu George Mpanda  anazalisha kazi zenye melody kali kitu kinachofanya wimbo kuwa na maisha marefu kwenye maiskio na akili za watu.

Moyo mashine ni wimbo wa kumwimbia ama kumdedicate kipenzi chako, kwa kipindi hiki anaweza toa chozi la furaha.
#BenPolumetunyoosha.
Niambie ulichokiona kwenye Moyo mashine ya Ben Paul, niandikie hapa chini.

0 comments:

Post a Comment