ads

Sunday 17 May 2015

KWA NINI ALIKIBA ALISHANGILIWA KWENYE FIESTA?

Na Moringe Jonasy
Hii ni mara ya tatu naandika juu Alikiba , hii inatokana na hali iliyopo hapa nchini kwa wapenzi wa bongofleva hadi wasiokuwa wapenzi kwani limekuwa jambo lililozungumziwa sana nchini kuliko hata suala la kuuawa kwa mlipuaji mabomu huko Arusha.
Japokuwa sikuwa Leaders ile jumamosi ,nilibahatika kuiona ile show online na kung'amua vitu vichache ambav
yo vilimfanya alikiba ashangiliwe sana.Mambo matano yafuatayo yanaweza kuwa sababu ya Alikiba kushangiliwa...

1.SAUTI YAKE
Kwa bahati nilikuwa miongoni mwa watu tuliofanmikiwa kumsikia Alikiba kabla ya Njiwa na Cindelela ambazo zilimweka kwenye ramani ya bongofleva kwenye wimbo mmoja ambao alikuwa ameimba na wasanii wenzake lakini sauti yake ilinifanya niupende ule wimbo waliouita Leila.
Kuna mtu mmoja aliniambia alikiba anabana pua nami nilimpa jibu rahisi tuu kuwa KAMA ANABANA PUA BASI ANABANA VIZURI. Lakini alikiba alithibitisha kuwa alikuwa akibana pua kabla hajaenda kuimba na R Kell ambapo alifunzwa jinsi ya kuimba vizuri huku matumizi makubwa ya koo , pua na ala nyingine za sauti na matokeo yake tuliyaona kwenye nyimbo zake kama Mapenzi,feal free ,Dushelee,my Everything na Mwana dsm ambazo zinazidi kutuonesha tofauti kati ya wasanii wa Marekeni na wa Bongo.
Hii haikumpa shida kuimba kwa sauti yake yenye ubora pale jukwaani na kuendelea kuibua shangwe kutoka kwa mashabiki wake wengine waliopo kwenye hili kundi la kutumia vyema sauti zao ni pamoja naMarlow ,Rama D na Diamond.

2.MWANA NI HABARI YA MJINI
Hili halina ubishi kuwa mwana ni miongoni mwa hit song kwa kipindi hiki , wimbo una sifa zote ujumbe, sauti na pia unachezeka.Ningeshangaa kama Alikiba angeshangiliwa kama angekuwa na my everthing kama silaha yake wakati alishatutibua wafuasi wake kwa kutotoa video. Kama ilivyo Mdogo mdogo ,Pacha wangu,Najiona Mimi na nyingine nyingi zinazotikisa jiji.
3.ALIVYOTINGA STEJINI
Alingia kwa mbwembe huku akiwaambia wafuasi wakiwa na hamu ya kuona kitu ambacho angekifanya baada ya kukaa kimya kwa muda wa takribani mwaka mmoja.Kama angekuwa hajarudi kweli nilitegemea kuwa angezomewa lakini kwa kuwa alikuwa amerudi kweli Shangwe ilikuwa haki yake.
4.HURUMA YA MASHABIKI
Mashabiki wamemhurumia Alikiba baada ya muda wa malezi na kumpa nafasi mdogo wake huku akijifanyia kautafiti juu ya mziki wetu akiwa nje ya hii tasinia.
Vimaneno vilivyozungumzwa wee na watu juu yake viliwafanya wafuasi wake wampe moyo na kumwambia kuwa anaweza na wapo pamoja naye.
5.KUMPA DENI
Kilichofanywa na mashabiki pale Leaders alikiba asikione kama ni ushujaa ama ushindi wa vita ambayo alikuwa ameshinda bila kuwepo kwa hiyo vita bali atambue mashabiki wamempa deni ambalo aanze kulilipa kwa kutoa video ya mwana Dsm yenye ubora,collabo la maana na wakali wa muziki Duniani lakini mwisho waje kumpigia kura si kwenye Kill bali kwenye kora,MTV,Chanel O , BET na nyingine nyingi.
NAOMBA KUWASILISHA NI MTAZAMO WANGU HUU

0 comments:

Post a Comment