ads

Saturday, 27 June 2015

DIAMOND NI WAKATI WAKO WA KUTOA ALBUM


Na.Moringe Jonasy
Kwanza nikupongeze baada ya kupata tunzo za muziki Tanzania kwa mara nyingine  baada ya mwaka jana kuweka rekodi ambayo ni vigumu sana kufikiwa na wasanii wengine wa muziki nchini.Lakini pia nikupongeze kwa kuchaguliwa kugombea tunzo nyingine za kimataifa kama za MTV na kwingineko ambako juhudi zako ukimtegmea Muumba zimekufanya uonwe huko nje na kuwekwa huko.
Ni hatua kubwa sana kuwekwa kwenye vipengele vitatu na hesabu kama ni ushindi maana kuna maelfu ya wanamuziki Afrika ambao walitamani hata kutajwa walau mara moja tuu lakini kwako ni mara ya pili.
Kwa kura za watanzania na wapenzi wa muziki wako nje ya Tanzania naamini una nafasi ya kushinda mbili ama moja kati ya tunzo unazoshindania japokuwa kuna uwezekano wa kushinda zote lakini kuna kipengele kimoja ambacho unashindana  na wanamuziki wakubwa zaidi yako Afrika hivyo ushindani utakuwa mkubwa sana ndiyo maana nina uhakika kuwa mbili zaweza kuja Tanzania kwa mara ya kwanza.
Ushindi wako ni ushindi wa mtanzania yeyote kwani kwa kushinda kwako utaifanyaTanzania kutazamwa kwa jicho la tatu kwa upande wa muziki kwani  kwa mtu mwenye akili hawezi kuamini kirahisi kuwa Tanzania ina mwanamuziki mmoja ama wawili  tuu wenye sifa ya kutambuliwa Afrika hivyo utakuwa umefungua milango ya mafanikio kwa wanamuziki wengine ambao wana kipaji sawa ama hata zaidi yako na kufika mbali zaidi.Nimekuwa mmoja wa wapiga kura hasa linapokuja suala la kitaifa kama hili wakati mwingine nimekuwa nikipiga hata kiushabiki tuu ili mradi mtanzania ushinde.Hata awamu hii nimekupa kura yangu na kumwacha Wizkid ambaye ukweli unanisuta kuwa bado kidogo kumfikia lakini nitafanya nini utanzania tuu unanisukuma.
Tuachane na habari za tunzo unazishindania, naomba tuongelee suala la wanamuziki hasa wa Tanzania kusita ama niseme kuogopa kutoa Album badala yake wamekuwa wakitoa nyimbo kwa kudonoa donoa wakikwepa kile wanachokiita wizi wa kazi zao.Ni kweli tumeshuhudia wamnamuziki wengi wakilia na jambo hilo na wenzetu wa filamu ndo usiseme wamebaki kulia kilio cha samaki na machozi kusombwa na maji , hakuna anaye wasikia na hata kama kilio chao kinasikika basi wakisikiao bado wanahisi kilio chao kama wimbo Fulani wa hisia ambao unawafanya wasinzie badala ya kuamuka na kuchukua hatua.
Wengi wanaogopa na wamejiapiaza kutotoa Album lakini kwa watu wa filamu watafanya nini zaidi ya kukubaliana na hali maana licha ya kazi zao kunakiliwa zimekuwa zikikodishwa.Lakini ninachojiuliza hakuna wanachokipata hata kidogo?
Jibu ni hapana.
Hivyo kuna wanachokipata licha ya kuwa hakilingani na walichotakiwa kupata ndiyo maana tunawaona ni miongoni mwa mabingwa wa kuuza sura mitandaoni na kwenye kumbi za starehe japokuwa kuna madai kuwa wana vyanzo vingine halali na haramu vya kujiingizia pesa.Vyanzo halali ni kama  mauzo ya kazi zao, malipo matangazo mbalimbali na kazi nyingine rasmi kama biashara na nyinginezo.
Kwa wanamuziki kama wewe una cha ziada kwani una matamasha ya ndani na nje ya nchi na kuuza kazi mtandaoni  na hata nyimbo zenu kutumiwa kwenye kampeni Fulani kama  vile vita dhidi ya madawa ya Kulevya,UKIMWI ukeketaji na hata kuhimiza kilimo japokuwa kwenye jambo la mwisho mmekuwa waoga sana kuandika kuhusu masuala hayo.
Sasa nini kinachowafanya muogope kutoa Album zaidi ya wizi wa kazi zenu kwenye zama za sayansi na teknolojia kama hizi?.Kama kuiba hata hizo nyimbo mnazodonoa donoa zinaibiwa licha ya kuuza kwa njia za kisasa maana pia kuna njia za kisasa za kuiba.Mfano ukitoa wimbo mpya nitaununua kisha nitawarushia wenzangu zaidi ya kumi kupitia parua pepe ,Bluetooth ama hata whatsap na hata ukiweka video youtube mwingine anaweza ipakua na kuanza kuiangalia na kuwatumia wengine kupitia whatsap hivyo kupunguza idadi ya watazamaji ambao wangekuwa kama kichocheo cha kulipwa na youtube ama hata google.Nasema haya kwa kutaka kukuambia hata kwenye kudonoa donoa kuna wizi hivyo naamini kama utatoa album utauza na kupata faida kubwa huku wizi nao ukiwa mkubwa.
Najaribu kufikiri Album yenye nyimbo kali kama my number one, number one remix, nana ,mdogo mdogo ,nasema nawe ,nimpende nani na nyingine nyingi ambazo hazijatoka kamaulizowashirikisha  wanamuziki wengine wa Afrika na nje ya Afrika itakuwaje Afrika na duniani ikiuzwa kupitia mitandao na kwenye CDs.Hautakuwa bilionea tuu kama siyo tirionea ama nusu tirionea.
Si pesa tuu itakuweka kwenye daraja Fulani la wanamuziki kwani licha ya kuwa na tunzo kubwa za muziki pia iadadi na mauzo ya album ni moja ya kipimo cha ukubwa wa mwanamuziki.Na hata kwenye kusaini na makampuni makubwa ya muziki kinachoangaliwa ni pamoja na idadi na ubora wa album ndiyo maana licha ya uwepo wa wanamuziki wengi wazuri kipindi Airtel one 8 project Alikiba alikuwa chaguo la kwanza kutokana na kuwa ni mwanamuziki aliyevunja rekodi za mauzo ya album Afrika mashariki.
Unaweza kuuliza kwanini Diamond , lakini ukweli ni kwamba wewe ndiye mwanamuziki unayeangaliwa zaidi ndani na nje ya Afrika  hivyo wanamuziki wengi wanakuangalia wewe kama mfano wao hivyo kama nawe utawatisha kama ulivyotishwa na watangulizi wako  basi tutaishia kudonoa donoa tuu vinyimbo vizuri huku mkitunyima haki yetu ya kusikiliza albuma ambazo amini usiamini zitakuongezea mashabiki kama siyo wafuasi ambao wanapeda kusikia nyimbo za mwanamuziki Fulani zilizokusanywa wakisikia ubunifu wako badala ya kusikia tuu nyimbo chache chache zitokazo kwa vipindi.
Lakini pia wewe ni mmoja wa wanamuziki wenye mafanikio makubwa  ndani na nje ya Afrika hivyo suala la kuingia mikataba isiyo ya kibabaishaji na makampuni yatakayoweza kukuibia ni gumu sana lakini pia una uzoefu na biashara ya muziki hivyo kuziba mianya ya wizi ni jambo jepesi kuliko kwa mwanamuziki mchanga kama Mo music kwa mfano.
Sababu nyingi ya kwa nini Diamond ni kwamba wewe ni miongoni mwa wanamuziki wachache wenye matamasha na ziara nyingi iwe nchini ama nje ya nchi hivyo ukiwa na album unakuwa na hazina kubwa ya nyimbo za kuimba jukwaani badala ya ufanyavyo sasa kuimba nyimbo za ablum ya kwanza nyimbo chache ulizozitoa karibuni.
Pia ablum hukutengenezea wafuasi wengi kuliko mashabiki.Unaweza jiuliza ni kitu gani hiki ila kwa kifupi mashabiki ni wale wanaokupigia kelele kukushangilia kwa si kwa sababu ya kupenda kazi zako bali kwa sababu nyingine ama mwonekano wako ama chuki dhidi ya mtu mwingine yaani akutumie wewe kupooa hasira zake juu ya huyo mtu anaweza akawa mwanamuziki, mtayarishaji na hata muigizaji lakini mfuasi yupo na wewe kwenye raha na shida zako.Mfano Alikiba ni mwanamuziki mwenye wafuasi wengi tangu kale kutokana na album zake alizozitoa awali, Juma nature naye hivyo hivyo kama ilivyo kwa Lady Jay Dee ,mwana FA ,Marlow ,Pro.Jay na wengine wengi  hii yote kutokana na album ambazo si tuu zinawapa nafasi ya kuburudika na kazi zako bali kuzieleewa zadi kwani kwa utafiti wangu usio rasmi ni kwamba ukisikiliza album Fulani hutoisikiliza mara moja bali utaisikiliza zaidi na zaidi na kuelewa hata kile ambacho kilicjificha kwenye talata yako tofauti na kusikiliza  nyimbo kwa misimu kutokana na upya wake.Ulifanikiwa kulifanya hili ulipotoa Album ya kwanza lakini ghafla ukasikiliza ya wakongwe badala yake unashabikiwa kwa msimu kutokana na upya wa kazi jambo ambalo si zuri sana kwa mwanamuziki mkubwa kama wewe ni wakati wa kutengeneza wafuasi sasa ufaidi matunda ya kazi zako.
Na sababu ya mwisho ambayo si ya kiuchumi sana bali ya kisanaa zaidi  ni kwamba Album ni kama kipimo cha kipaji chako.Nikupe mfano mmoja wapi alipo Sam wa Ukweli? Unaweza usijue kilichompoteza ama  unaweza nipa sababu nyingine za kawaida kufikiria.Ila ukweli ni kwamba Sam mmoja wa wanamuziki ambao niliwatabiria makubwa kama nilivyofanya kwako amemezwa na mafanikio ya album yake ambayo kiukweli ilikuwa ni bora.Yupo kama amemaliza kipaji chake kwenye ile Album yaani alifikia mwisho wa kufikiri na kwa kutoa ile album hivyo hata akija kuimba anaweza kurudia idea za kwenye ile album kama alivyofanya kwenye kurudia namna ya uimbaji kwenye ile album yake.Hivyo ukitoa album zaidi na zaidi kipaji chako kinapimwa haswa na kukubalika zaidi.Au unafanya ulisema kwenye spora show, kuwa  haiwezekani mwaka mzima ushindwe kutunga wimbo mmoja mzuri? Kwa hiyo itakuchukua mika zaidi ya kumi kuandaa album nzuri?.
Naomba niishie hapa nikikusisitiza kuwa huu ni wakati wa Diamond kutoa album ya pili.
Naomba kuwasilisha #mwanakalamu.

0 comments:

Post a Comment