ads

Saturday, 4 July 2015

CHEKECHA CHEKETUA VIDEO NA NADHARIA ZA UHAKIKI


Na.Moringe Jonasy Mhagama
Uhakiki ni kitendo cha kutathmini ,kueleza ,kuainisha  na kutoa maoni juu ya kazi Fulani ya fasihi kwa kuongozwa na kaida maalum.Kazi hiyo ya fasihi inaweza kuwa; shairi,hadithi tamthilia na vipera vyake.
Kumekuwa na mjadala mkubwa sana juu ya dhana ya uhakimki wa kazi hizo za fasihi na kutengeneza makundi makuu mawili kundi la kwanza likidai kuwa  mwandishi ama mtunzi ndiye ajuaye dhima na muundo wa utunzi wake kwani hujua kilimchochea kutunga hiyo kazi na kundi la pili likidai kuwa kuna haja ya watu wengine kueleza, kuainisha na kutoa maoni juu ya kazi hiyo kwa kuzingatia mambo mbalimbali kama itikadi,historia ,tamaduni na hata imani ya mtunzi wa kazi hiyo.
Kundi la kwanza linaamini kuwa kuna uwezekano wa kuchambua umbo  la nje na ndani mwa kazi hiyo ya kifasihi lakini kuna vitu ambavyo mtunzi anahitajika kutoa alichokimaanisha na kundi lingine limeweka misingi mbalimbali ambayo itawaongoza wachambuzi wa kazi hiyo.

Turudi kwenye mada yetu ya leo kuhusu video ya chekecka cheketua ya mwanamuziki Alikiba ambayo haijamaliza wiki moja tangu itambulishwe kwote duniani.Kama ilivyokuwa mwana wengi waliikosoa na kudai si nzuri na bilinganya kibao ili mradi tuu kutoa kasoro.Bahati mbaya wengi walioikosoa walishindwa kutoa sababu anata waliotoa sababu walikuwa na sababu nyepesi sana hali iliyomfanya hata Alikiba mwenyewe awaone ni ‘’wenye chuki binafsi tuu’’.Kabla sijaamini kuwa alikuwa ni watu wenye chuki pekee ndio waliikosoa ile video ngoja niandike mambo yafuatayo juu ya nilichokiona kwenye wimbo ule.
1.WIMBO KUTOELEWEKA KWA WENGI MWANZO
Haujaimbwa kwa lugha ambayo haitumiki Tanzania, mashairi yamebeba maneno ya Kiswahili  na machache sana yalikuwa ya iingereza kama siyo neno moja .Wengi waliposikia jina la wimbo hawakujua ni wimbo wa aina gani na hata ulipotoa wengi walionekana kutouelewa hadi pale walipomwona akitumbuiza jukwaani hapo ndipo walipoanza kujenga maana yao ya wimbo huo, walikiona kiitikio kilichokuwa na maneno matatu yaliyojirudia rudia ndiyo dhana kuu ya wimbo na kuhisi hata video yake itatawaliwana wasichana wenye kile AY anakiita ‘’zigo’’ wakishindana ‘’kucheketua’’ kitu amabacho si sahihi kwani wimbo ulibeba dhana pana zaidi ya kucheketua.
Wengi walitegemea video ingewapa maana halisi lakini walipokutana nayo walijikuta wakisema mbaya mara mpangilio wake mbaya mara uchezaji mbovu na mambo mengi yenye uhai mfupi kuliko njiti ya mwisho ya kiberiti.
2.UPEKEE WA ALIKIBA KATIKA UTUNZI
Alikiba ni miongoni mwa watunzi wa kipekee ambao wanauandishi wakipekee sana hapa nchini, akiandika hadithi kwenye wimbo basi maneno na misemo atakayoitumia basi itamfanya msikilizaji atake kusikia tena na tena alichokiimba rejea Mac Muga ,Dushelele,Hadithi na hata mali yangu ni simulizi zenye ufundi wa hali ya juu.Namana yake ya utunzi ndiyo iliyowafanya wengi kutoa tafsiri ya ziada kweye wimbo wake wa ‘’Mwana’’ Kwani walishazoea kuwa huyu mtu huandika kwa kutoa maana zaidi ya maana ya mwanzo.
Upekee huu wa kiuandishi ndiko kulikopelekea wengi waachwe njia panda kwenye video ya chekecha cheketua ambayo imezingatia tyuni , marimba na maana ya mashairi yake hili linaonekana kwenye madhari ya video na hata mwonekano wa wahusika wa  kwenye video.
3.VIDEO KUWA NA ZAIDI YA KISA KIMOJA
Tofauti na kwenye video za nyimbo zilizotangulia kama vile Hadithi,Karim, Mac Muga na hata mwana ambayo mwimbaji huyu aliamua kutamba mashairi yake na kucheza sehemu ndogo ya wimbo wake akiheshimu kile mwandaaji wake na mpiga gitaa  kwenye chekecha cheketua Ally aliamua kuweka viza zaidi ya kimoja kitu ambacho wengi hajaking’amua.Kuna kisa cha yeye (Kiba) Yule mrembo ambaye yupo na mama yake na hata Yule kijana mwingine.Wengi wamechanaganya visa na kuiona video haieleweki na wengine wakaenda mabli na kudai haina maana.
4.KUHESHIMU NA KUSIKILIZA  ALA ZA MUZIKI
Hapa marimba,gitaa , ngoma , zumari na vinginevyo vinahusika.Alikiba ameendelea kuwa mtumwa wa gitaa si tuu awapo jukwaani bali hata kwenye video zake ( rejea mwana ).Hiki pia amaekifanya kwenye video ya chekecha cheketua Ally amesikiliza marimba  kuandaa ‘’script’’ ambayo imekuwa ya kiasili zaidi kuanzia usela ,uchezaji na hata madhari ya video angekuwa wa ajabu kama asingezingatia hilo na kujaza meli ndege na maghorofa kwenye wimbo wa aina hii japokuwa kwa wengi wanaoangalia muziki kwa juu juu wangemsifia na kumwona amepiga hatua kumbe angerudi nyuma hatua nyingi sana maana hicho kitu tumekiona kwenye nyimbo nyingi sana.
5.KULINGANISHA VIDEO HII NA ZA WENGINE
Hii ni kasumba kubwa ambayo wengi tunakosea na kujipa uhuru wa kuona hiki kitu si sahihi ama kibaya.Kuna mahali kweli panahitaji kulinganisha ambapo ni kwenye ubora wa video ambako kwa mwanamuziki kazi yake ni kutoa pesa  kwa mwongozaji ambaye naye kufanya kazi.Lakini tumekuwa tofauti ubora twaukubali lakini visa hatujavielewa basi tunaropoka tuu eti ‘’mbaya’’Japokuwa binadamu hana asilimia mia ya utendaji ‘’efficient’’ lakini wengi wanataka visa viwe kama vya wanamuziki Fulani ama wa Marekani ama hata ulaya ambao kwao  wanaona kama wakuwaiga.Kweli kuiga tuige vingine lakini si kwenye sanaa ambako mtunzi ndiye mmiliki wa kitu hicho.Mfano kama Eric shigongo anaandika hadithi za namna Fulani akakubalia si lazima wote tupite njia hizo ndipo tutafika alipofika Eric hicho ni kipaji ambacho ni kama uumbaji mwingine mfano ng’ombe wanaweza kufanana rangi na hata urefu wa pembe lakini unaweza kutofautisha mmoja na mwingine ndivyo vipaji vyetu.
KWA MASHABIKI NA WAPENZI WA MUZIKI
Mwisho niseme kuwa video ni nzuri kwa yule amabaye ataamua kuhakiki kwa kufuata nadaria yoyote ya uhakiki bila kutanguliza ushabiki. Si mbaya kama wengi wanavyotaka kutuaminisha bali mambo niliyoeleza hapo juu yamechangia  kuleta maneno hayo bahati mbaya wengine wameangalia video mara moja halafu wanatoa hukumu bila kujua mwanamuziki huyu amevumbua nini na kukiweka kwetu.Wengine wamefika mbali hata kuanza kumtusi na kumwona mtu wa ‘’level’’ zao ,wengine wameenda kwenye ukurasa wa TRACE Nigeria na kuanaza kutoa maneno ya shombo mara ehhee sijui video imesambaa sana whatsap na aliyeisambaza ni yeye(Ally) hivyo haina ule upya kama walivyodai Trace.Huenda kweli video ilisambaa ila wengi hawajua kuwa hawa wanamuziki huwapa watu wao wa karibu , wanamuziki wenzao na hata waongozaji wa hapa ndai kutoa maoni yao kabla ya kuitambulisha kwa hadhira hivyo watu hao wanaweza kuisambaza kwa watu wengine wanaowaaamini kisha kusambaa sasa hayo maneno yana malengo gani kama siyo chuki?.
Lakini video hii pia imewafanya wengine waendeleeze kile wanachokiita ‘team’ amabazo kwa bahati mbaya hazina msaada nchini bali kuiaibisha nchi kwa kutunana sisi kwa sisi na kuwatukana wazazi wetu wengine wka bahati mbaya ni marehemu.Timu hizi hazina ile maana ya timu halisi kwani hakuna timu popote duniani yenye kazi ya kumshusha Fulani  na kumpaisha mwingine hata kama hastahili kupaa.Timu hizi zinafanya kazi kinyume kabisa na maana halisi nijuavyo timu huundwa ama hutokea kwa malengo chanya lakini kwetu ni shaghala baghala.
USHAURI WANGU KWA ALIKIBA.
Ni kutopishanisha wimbo na video yake kwa muda mrefu sana kama ilivyofanyika kwa wimbo huu japokuwa kulikuwa na sababu maalum zilizochelewesha zaidi video.Kama asingetoa wimbo hata matatizo yaliyokwamisha yasingemuathiri hivyo naamini atakuwa amejifunza na kama atatoa wimbo pekee basi iwe kama bonas tuu baada ya kutoa video na wimbo mpya na si kufanya alichokifanya.Naamini wasimamizi wake wamelijua hili na sitegemei kama litajirudia tena.
Pia kwa video hii ajaribu kuongea kwenye chombo chochote maana ya kazi hii ya chekecha cheketua ili awatoe gizani ambao hawajaielewa kwani wahakiki huru wamegoma kufikiri zaidi na kutuaibisha watanzania.

0 comments:

Post a Comment