Na.Moringe
Jonasy
Habari
wanakalamu mwenzangu, poleni na majukumu ya kila siku ,wengi wamekuwa wakifuatilia
kilichokuwa kikiendelea Dodoma najua sahizi mambo yanaendelea kama kawaida.Ni
kitu kizuri sana kujua hata kinachoendelea kwenye siasa za nchi yetu na jambo
la msingi sana ni kwenda kujiandikisha ili kupata kitambulisho
kitakachotusaidia kupiga kura kwani ni hai na wajibu wetu kama watanzania wenye
sifa za kupiga kura.
Wakati
mchakato ukiendelea Dodoma mjadala ulikuwa mkubwa sana na nilibahatika kukaa na
wenzangu tukijadili hili na lile juu ya sifa ya kiongozi tunayemwitaji
watanzania kwa sasa mojaya sifa ambayo ilikuwa kama imebeba mambo mengi kama
siyo yote ni ''UZALENDO'' .
Je,
tunajua maana ya uzalendo?
Nani
anatakiwa kuwa mzalendo?
Kivipi
unaweza kuwa mzalendo?
Unaweza
kunufaika na uzalendo?
Je,
kama hakuna uzalendo kuna nini kinachoweza kutokea?
Hayo ni baadhi ya maswali niliyokuwa nikijiuliza baada ya kutoka kwenye mjadala huo ambao uliisha kwa kila mtu kutoa lake analolijua.
Uzalendo
umefasiliwa kwa ujumla kumaanisha ‘mtu kuwa na utiifu, upendo na kujitolea kwa
taifa au nchi yake’. Hii inamaanisha kuwa, kila mwananchi wa nchi fulani
anapaswa kuweka maslahi ya taifa lake mbele kwa kila akifanyacho kwa kuzingatia
kuwa kila alitendalo linamwathiri kwa namna moja au nyingine mwananchi
mwenzake, ambae ndie dada, kaka, mama na baba yake.
Uzalendo
umejikita zaidi katika matendo na si maneno matupu tu. Matendo hapa yanahusu
wakati wowote ule, iwe wakati taifa likiwa katika dhiki au furaha. Dhana ya
uzalendo inajipambanua zaidi kuwa kwa mzalendo, kuitumikia nchi yake kwa
uaminifu na kwa manufaa ni fahari kubwa kupita zote.
Wanapozungumzia
uzalendo, Wamarekani hukumbuka zaidi msemo wa Patrick Henry alioutoa wakati
wakipigania Uhuru wao dhidi ya wakoloni Waingereza kuwa ‘give me liberty or
give me death’. Kwa tafsiri siyo rasmi, Henry alimaanisha kuwa katika
kupigania nchi yake, mtu awaye yote hupaswa kuchagua moja tu kati ya mambo
mawili ‘kupata ukombozi au kifo’. Tunayosimuliwa jinsi Chifu Mkwawa wa Wahehe
alivyopinga ukoloni wa Wajerumani hata kumgharimu maisha yake yanaakisi kauli ya
Henry.
Msamiati
ama neno Uzalendo limekuwa likitumika kwenye nyanja mbalimbali Muziki ukiwemo
hasa pale myuziki ama mwanamuziki anapovuka mpaka wa nchi.Haikuwa ajabu BASATA
walipomwonya Shilole kwa madai ya picha yake kusambazwa mitandaoni akiwa kwenye
mwonekano usio wa kimaadili.Na taasisi hiyo ilienda mbali na kudai kuwa kila
mtanzania hususani wanamuziki wanapopata ziara ama matamasha nje ya nchi hupewa
kibali na huwa wamebeba utambulisho wa Tanzania kama taifa hivyo kwa kufanya
kitendo kilichokuwa kinyume na maadili yetu kilitafsiriwa kama udhalilishaji
kwa taifa.
Uzalendo
ulikosekana kwa mtu kuangalia hisia zake zaidi badala ya utaifa aliokuwa
amevikwa ndiyo maana akapewa onyo lile.
Si
hivyo tuu imetyokea pia wanamuziki ambapo wamekuwa wakiliwakilisha taifa si tuu
kwa kushiriki kwenye tunzo za kimataifa bali hata kutumbuiza kwenye matamasha
ya kimataifa na yasiyo yakimataifa nje ya nchi.Kufanya kwao vyema kunalipaisha
taifa na letu.
Wanamuziki
mbali mbali , wasanii mbalimbali na waigizaji hapa nchini wameliwakilisha taifa
kupitia kazi zao miongoni mwao kwa kuwataja wachache ni AY,Juma
Nature,Marehem,u Steven Kanumba, Wema sepetu, Jakate mwengelo,Vanesa Mdee, Lady
Jay Dee, Diamond ,Fid Q, Saida Karoli, Aslay, shaa, Joh makini , Alikiba , Martin
Kadinda, Sheria Ngowi, Peter Msechu na wengine wengi kufanya kwao vizuri
kuliwafanya waliwakilishe taifa letu vema na wameonesha uzalendo wao kwa kujituma na kutofanya vitu vilivyopoteza
ma kupunguza heshima na hadhi ya taifa letu.
Sasa
wakati nafikiria nafasi ya kila mtu kuwa wazalendo kwa taifa lao wakiwemo
wasanii na watru wengine maarufu nikakumbuka hili linaloendelea kwenye tasnia
ya muziki nchini ambapo baadhi ya wanamuziki wakitajwa kama si wazalendo.
Alikiba
ni mmoja wa wanamuziki amabo wamedaiwa kuwa si wazalendo kwa kuwapa nguvu
wanamuziki wanaoshindania tunzo za uziki nje ya nchi kufikia hatua ya waandishi
wa habari kumuuliza alipokuwa kwenye moja ya kituo cha redio nchini.Nilipenda
majibu ya Akiliba kwani yalifichuo uozo na ujinga wetu juu ya dhana ya
uzalendo.
Alijibu
kuwa alikuwa ametoa matangazo mbali
mbali kupitia kwenye account yake ya Instagram kwa wanamuziki waliokuwa
wamemwomba kufanya hivyo.Laki Ally alinda mbali kwa kugeuzia kipao upande
mwingine kwa kuhoji kwa nini amekuwa akiulizwa yeye kuwafanyia wenzake kuonesha
uzalendo wakati kuna aliokuwa ameomba wenzake kutangaza kazi zake za kapeni ya
kutokomeza Ujangili ambayo yeye pamoja na watu wengine wamejitolea kufanya kazi
hiyo ambayo si jambo dogo na linagusa utaifa zaidi si kwa faida yake pekee, na
walioitikia wito huo walikuwa ni watu wachache tofauti na aliokuwa amewaomba.
Ilishangaza
kwa jambo ambalo linagusa taifa kwa kiwango kikubwa likipuuzwa na kubezwa kwa kulazimishwa
kumtangaza mtu amabaye hakuona hata umuhimu wa kumwomba amuwekee tangazo lake
la kuomba kura kwenye tunzo za kimataifa kutumia neno Uzaledo hapo ndipo
maswali yangu ya pale juu kuhusu uzalendo yanahitaji majibu.
Nani
anapaswa kuwa mzalendo, Kwa nini na kwa wakati gani? Na maswali mengi amabayo
najua wengi tunayajua bmajibu yetu lakini kwa kujifanya vipofu na viziwi
tunaimba wimbo wa uzalendo kwa manufaa ya hisia zetu.
Sikatai
kumekuwa na sintofahamu kwa wanamuziki hawa ambayo daima nimekuwa nikisisitiza
kuwa inakuzwa na wanahabari na washabiki kwa kujua ama kutokujua lakini kwenye
masuala yanayogusa maslahi na sifa ya taifa hili lilikuwa ni jambo la kuweka
pembeni sifa binafsi.
Nilishangaa
pale watu waliohoji Ally alipomwombea kura Mwanamuziki kutoka Nigeria na
kumwacha mwanamuziki kutoka Kenya au Uganda bila kujua kuwa kipengele hicho
kilikuwa cha video bora na ile video ulikuwa imeongozwa na mwongozaji aliyeongoza
video yake mpya iliyotoka karibuni Chekecha cheketua.
Ingekuwa
kwenyekipengele hicho kulikuwa na mwogozaji ama mwanamuziki wa Tanzania hapo
ningemshangaa sana Ally kama nilivyoshangaa hao wanaoudai Uzalendo kwa Ally
wakimwacha Diamond ambaye licha ya ukubwa wake Afrika hakuutumia uzalendo
kutangaza ujio wa video mpya ya Alikiba na kumtangaza zaidi Alikiba kutokana na
kuwa na washabiki wengi ndani na nje ya Afrika pengine kuliko mwanamuziki
mwingine nchini.
Uzalendo
unaongelewa wa kumtukana mwanamuki wa ndani kwenye ukurasa wa kituo kikubwa cha
televisheni Afrika na duniani ni
uzalendo wa aina gani?
Inashangaza
sana tunapotumia neno uzalendo kuwatuhumu wenzetu na kujisifia bila kujali mantiki yenyewe ya neno uzalendo.
Kwa
mantiki hiyo UZALENDO unakosa maana kutokana na matendo yetu na ubinafsi wetu
kama wafanyavyo wanasiasa na watu wengine wengi wakifanya mambo yanayopoteza maana ya neno uzalendo.
Niambie
#mwanakalamu mwenzangu
0 comments:
Post a Comment