Na;Steven Mwakyusa (Mtu Makini)
Katika muziki wa bongofleva kumewahi tokea wasanii ambao walihit
katika nyimbo walizoshirikishwa na baadaye watu wakawa na hamu ya
kuwasikia katika nyimbo zao wenyewe, ila matokeo yake yalikuwa tofauti!
Ebu tujikumbushe wasanii waliong'ara katika nyimbo walizoshirikishwa na baadaye wakashindwa kusimama wenyewe!!
1. Mishi- Huyu kwa mara ya kwanza alisikika katika wimbo wa Selina wa
Alicom, baadaye akasikika katika Chonde chonde ya Nuruel, Pole kwa
safari ya Juma kakere pia Nimeridhika naye ya Qchief, baada ya hapo sina
kumbukumbu kama aliwahi imba wimbo wake mwenyewe achilia mbali kusikika
katika collabo nyinginezo!!
2. Zahran-Huyu ni msanii aliyesikika
na kufahamika katika wimbo wa Abby Skills(Nilikupenda), baadaye alikika
katika Sikuoni ya Alikiba, baada ya hapo ni kimya mpaka leo!!
3.
Lil Gheto-Huyu kwa mara ya kwanza alisikika katika wimbo wa Ji(Kidato
kimoja), baadaye alisikika katika nyimbo za Berry Black na AT, na mpaka
leo hajawahi tengeneza hit yeyote kama Solo artist!
4. Scount
Jentaz-Hawa kwa mara ya kwanza walisikika katika nyimbo za DNF, huku
Jirushe(Original version) ikiwapa jina mjini kwa kipindi hicho, mwisho
wa DNF ukawa mwisho wa SJ pia huku wakiwa hawajatengeneza hit yeyote!!
5. Miss Sarah- Huyu naye alisikika katika wimbo wa Caz T, Nakuhitaji (Angwisa), baada ya haoo hakuweza tena kusimama mwenyewe!!
6. Simple X- Huyu alisikika katika hakuna noma ya Prof J pia katika
Nawakilisha, baadaya ya hapo haijulikani aliimba nini tena!!
Wengine ni pamoja na
-Josephine-Kibanda cha simu(Soggy)
-Aliyeimba chorus ya Tumbo Joto(Kali P)
0 comments:
Post a Comment