ads

Monday 17 October 2016

REMIX ZILIZOFUNIKA NYIMBO ZA AWALI

Muda nwingine katika muziki inatokea msanii akafanya kazi ambayo anaamini ni bora kwa viwango vyake ila baada ya kutoka anakuja kugundua kwamba kuna vitu vinamiss!! Inaweza kuwa ni beat au kukosekana kwa vionjo fulani!
Huko nyuma imewahi tokea nyimbo original zikafunikwa na remix zake, remixes ziligeuka kuwa hitsong huku original version zikibaki hoehae...huku wengine wakishindwa kujua kama kuna original version ya wimbo husika!
Hizi ni baadhi ya nyimbo ambazo remix zake zilitamba zaidi ya original version..
1. Nikipata wangu-K_Lyn
Baada ya kuvuma na wimbo wa Nalia kwa furaha ambao alimshirikisha Bushoke, K lyn alijaribu kutoka mwenyewe akiwa na kibao kilichokwenda kwa jina la nikipata wangu, Hii nikipata wangu haikuweza kufanya lolote kumtangaza katika anga la muziki, baada ya muda ikaja kusikika remix yake akiwa mkali J-moe! Jmoe kwa kiasi kikubwa aliifanya nikipata wangu kuwa hitsong!!
2. Nipo Gado-Zay B feat Inspector Haroun
Hii ndiyo original version ndani yake alisimama Nyago ya mdizi Inspector Haroun Babu, licha ya ukali wa original version ila haikufua dafu mbele ya remix yake ambayo alikuja kusimama Juma Nature almaarufu kama Sir Nature aka Kibra..
Ikiwa katikati ya vuguvugu la beef la Nature na Babu, Nipo Gado remix iliweza kuhit na kuvunja rekodi za gado original.
3. Jirushe-Feruz feat Scout Jentaz
Wakiwa washirika wa karibu wa Daz Nundaz,Scout Jentaz walipata bahati ya kuwepo katika original version ya Jirushe na kufanya vizuri kadri ya walivyoweza!! Jirushe ya Feruz na SJ baadaye haikuweza kufurukuta mbele ya remix ambayo alikuja kusimama rapa mahili kwa kipindi hicho aliyejulikana kama Jmoe, Jmoe ndiye aliyefanya Jirushe iliyoanza kupoa ianze kupigwa kila kona ya nchi, vikorombwezo vya Intro pia outro aliyosimama Solo thang Ulamaa ilifanya Jirushe Remix kuwa wimbo bora kabisa kwa wakati huo.
4. Dochi-Imani
Ikiwa ni kazi toka Mj Records chini ya utayarishaji wake Marco Chali, Original version ya Imani haikufanya lolote mpaka ilipokuja kufanyiwa remix ndani yake akiwemo msanii nguli wa Bongo Flava Alikiba, uwepo wa sauti ya Alikiba ndani ya wimbo wa Imani ilifanya uanze upya kuchezwa huku wengi wakiamini ndiyo iliyokuwa original version
Kuna nyimbo nyingi sana zimefanyiwa remix mpaka sasa, nyingine zikiharibiwa huku nyingine zikiwa bora zaidi!!
Je unafikiri ni remix gani nyingine ambayo iliweza kuhit zaidi ya original version?


Steven Mwakyusa 2015

0 comments:

Post a Comment