ads

Wednesday 21 December 2016

ALIKIBA KAFANYA KILE WASICHOKIAMINI

Na.Mtu Makini
Mara nyingi sisi binadamu tumekuwa hatuamini katika kinachoitwa "Second Chance"
..Wengi tumekuwa tukiamini kwamba jambo likipita na mtu ukashindwa basi hakuna namna nyingine ya kulifanya likawezekana! Wengi tumekuwa na misemo kama "yule muda wake ushapita" "huyu alikuwa zamani" kwa sasa hawezi kufanya kitu! Hii imekuwa ikikatisha tamaa watu wengi na kuhisi kwamba hawawezi sahihisha makosa ya zamani, na pengine hawawezi kufanya zaidi ya wanavyofanya walivyofanya!

Msanii wa Bongo fleva ajulikanae kama Alikiba baada ya kukaa kimya katika muziki kelele nyingi zilipigwa za kumtaka arudi, naye bila hiyana aliitikia wito wa mashabiki na July 24 ya mwaka 2014 aliachia single mbili "Mwana" na "Kimasomaso"!
Single ya Mwana ilipokelewa vizuri kila kona ya na nje ya mipaka, huu ukawa mwanzo mpya wa safari ya kimuziki ya AK...wengi walimtia moyo na yeye akasonga mbele! Hapa kelele zikaanza kusikika kwamba AK alikuwa zamani, kwa sasa AK si chochote na AK alikuwa yule wa Cinderella..na hawezi kufika popote kwani muda wake umeshapita, hapa kuliibuka watabiri wa kila aina wakitabiri kusgindwa kwa AK!
Haikupita muda video ya Wimbo wa Mwana ilitoka, huku ikiwa ni video bora kabisa kwake kuwahi fanya toka aanze muziki..hapa kundi la watu likaibuka na kudai video ni mbaya sana, amebugi na haitafika kokote..tabiri zikaendelea ila video ikachezwa ndani ya Tanzania, Afrika na mpaka vituo vya Tv vya Ulaya huku mpaka sasa video ya Mwana ikiwa na viewers 9m+ youtube!
Mwaka huo huo wa 2014 wimbo wa mwana Ulimwezesha kupata tuzo 6 katika tuzo za KTMA...huku collabo yake na Mwanafa "kiboko yangu" ikipata tuzo ya collaboration bora kwa mwaka huo! Mayowe yakaendelea kupigwa kwamva AK hakustahili zile tuzo!!
Baada ya hapo akatoa single nyingine "chekecha cheketua" wimbo ambao ulihita ndani ya masaa 24, ni wimbo ambao ulivunja rekodi ya mkito katika kupakulia na kusababisha mtandao kuzidiwa, lakini bado watu hawakulipenda hili..tena wengine ni miongoni mwa waliomtia moyo wakati anaianza safari, tabiri zikaendelea kwamba hakuna lolote atakalofanya baada ya hapo, wapo walioanza kusifia wimbo wa mwana na kupinda Chekecha cheketua. Baada ya video kutoka maneno yakawa yale yale kama ya video ya mwana!

Baada ya hapo ilisikika Lupela ambayo nayo ilipondwa sana, si video wala si audio..hapa watabiri wa mambo wakawa wanajaribu kuhitimisha tabiri zao!
Baada ya Lupela ilikuja kutoka "Aje" hii ni kama ilikuja kukata ngebe za walio wengi, wale wakosoaji walishindwa nini cha kukosoa kuanzia audio mpaka video...Aje ikawa si wimbo tu ila ni zaidi ya wimbo, sasa ni takribani miezi 6 toka wimbo huu utoke ila uweza kumpa Alikiba tuzo 11 zikiwemo "Best African Act za MTV pia African Oscars..AK ameendelea kupata nomination lukuki kuanzia mitandaoni mpaka katika tuzo za vituo vya redio na TV...

Ni ndani ya mwaka huu AK alisainiwa katika lebo kubwa kabisa duniani "Sonny music" huku pia akipata ubalozi wa Wildaid!!


Ni mwaka 2016 ambao AK kafanya collabo nyingi zaidi na kuwatambulisha katika game hata ambao walikuwa wamesahaulika! Zile kelele kwamba hatofika popote ihali bado zinaendelea yeye kila siku amekuwa akiwaza kwenda mbele
Kwa uchache huu mwaka kafanya collabo hizi ambazo zote zimefanya vizuri na zinaendelea kufanya vizuri..
1. Unconditionally Bae_Saut Sol
2. Jike shupa_Nuhu Mziwanda
3. Mboga Saba_Mr Blue
4. Nisamehe_Baraka da prince
5. Averina_Abby Skills
6. Kajiandae_Ommy Dimpoz
7. Nitulize_Brown Mauzo
Hivyo basi naweza kusema 2016 ni mwaka ambao umempa mafanikio makubwa AK tofauti na matarajio ya wengi!
Na mwaka unaokuja naamini kuna mengi zaidi toka kwa AK, watabiri wa mambo nafikiri huu ni wakati wa kufuta zile tabiri zenu maana nina imani zitaendelea kuwaumiza kila kukicha!!

0 comments:

Post a Comment