ads

Tuesday 17 January 2017

MEDA CLASSIC ACHANA NA DIAMOND FANYA YAKO


Na;Mwanakalamu
Huenda nilichelewa kumsikia huyu mkali aliyeweka makazi yake kwa muda mrefu mjini Iringa, kwani nilianza kumsikia baada ya kuandika na kuimba kibao matata kilichoenda kwa jinala ''Barua kwa Diamond''.Kwa haraka haraka nikadhani ilikuwa njia ya kutaka kutoboa kwa kupitia jina la mwanamuziki ambaye alikuwa akitambulika ndani na nje ya Afrika ya mashariki.


Lakini inawezekana nilikuwa nimekosea kwani licha ya ukali wake wa maandishi na uimbaji na kuandika nyimbo kadhaa kali ambazo zingeweza kumtambulisha kama Meda Classic mwanamuziki mwenye kipaji kikubwa cha kuimba, kwani niliendelea kumsikia na kumwona akiimba na kuonekana kama 'kivuli cha Diamond' kuanzia mwonekano wake hadi kuimba nyimbo nyingine ambazo zilikuwa ni kama za kuonesha tuu namna gani anapenda uimbaji wa bwana Diamond.
Baada ya ngoma kadhaa ambazoo ni kama zilipuuzwa tuu na vyombo vya habari vya nje ya kanda ya kusini hususani Iringa Mbeya na Njombelicha ya ubora wake , nyimbo kama Kongoi,I love you,Somebody,Alele, na wimbo wa mrembo wa uswazi alioshirikiana na Nasi alijikuta akiendelea kuimba nyimbo za kumpaisha zaidi Diamond badala ya kumweka zaidi yeye juu.


Alikuja kuimba wimbo mwingine wa ''Princes Tiffa'' na sasa Kokoro remix ambazo licha ya kuzitendea haki kwa kuzifanya kwa ubora wa hali ya juu bado haziweza kumweka pale alipokuwa akitegemea.
Meda nakiona kipaji chake lakini naona kinapuuzwa na kuonekana na mwanamuziki mdogo na wakawaida kwa kuwa bado wengi wanakuchukulia kama shabiki tuu wa Diamond anayeamua kuimba nyimbo kujifurahisha na kuwafurahisha mashabiki wengine na si mtu mwenye mikakati ya kuwa Diamond mwingine ama Meda Classic mwanamuziki mkubwa.
Mwanakalamu nakushauri achana na Diamond fanya yako , wewe ni mkubwa na utakuwa mkubwa zaidi ya huyo unayefuata njia zake kama tuu utajua nini unakitaka.

0 comments:

Post a Comment