ads

Friday 2 June 2017

CHADEMA NA CCM TAFADHARI MSUBIRI KUWAPONGEZA WASHINDI




Na.Mwanakalamu.
Ni vigumu sana kalamu yangu kuandika mambo yahusuyo siasa,si kwa kuwa hazina umuhimu bali nimejikuta napenda sana kutumia kalamu yangu kuandika kuhusu fasihi ambayo inajitosheleza.Siasa ni maisha , siasa ni haki,siasa ni imani, siasa ni uhai kwa kifupi siasa ni kila kitu hivyo ina umuhimu mkubwa.

Kwenye dola yoyote kama siasa hazipo sawa hivyo vitu nilivyovitaja hapo juu huwa mashakani.
Palipo na siasa mbovu, vita hutokea,njaa huja, dini hazistawi, umoja, mshikamano na udugu havina nafasi na umasikini hutamalaki.Siasa safi ni moja kati ya nguzo za maendeleo ya jamii yoyote , hivyo siasa ni muhimu sana kwa maisha ya kila binadamu na kila mmoja anayo nafasi ya kuhakikisha jamii yake inaogelea kwenye siasa safi kwa ustawi wa jamii yake.
Baada ya kueleza kwa kifupi juu ya umuhimu wa siasa safi katika jamii yoyote, nirejee kwenye kile ambacho kimenifanya nishike kalamu yangu leo.Siku chache zilizopita nimeshtushwa kumsikia Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Upinzani nchini Ndugu F.A. Mbowe kuwa anatamuunga mkono Rais Uhuru  Kenyatta  wa Kenya katika uchaguzi unaotarajiwa nchini humo.Alienda mbali na kueleza sababu za kumuunga mkono Rais huyo Kenyatta kuwa ni moja kati ya mfano wa viongozi wa kidemokrasia aliyeruhusu uhuru wa kisiasa kupitia bunge na mikutano mingine ya kisiasa.
Lakini kwa taarifa  nyingine ambazo nimezisikia kutoka kwenye vyanzo vyangu vya kuaminika sababu hiyo imekuja baada ya urafiki wa Rais wa Tanzania na mpinzani mkuu wa Rais Kenyatta katika uchaguzi huo ndugu Raila Odinga.Urafiki huo umetafsiriwa kama msimamo wa Chama cha Mapinduzi.
Hiii imenitia shaka kwani siku chache baada ya msimamo huo wa Chama kikuu cha Upinzani nchini kupitia Mwenyekiti wake, ilitoka ripoti kutoka shirika moja la kimataifa juu ya ukwiukwaji mkubwa wa haki za waandishi wa habari nchini humo, uliohusisha kupigwa na kuumizwa kwa waandishi wa habari.Taarifa ilidokeza kuwa ‘mabloga 20’ wamepigwa na kuteswa kutokana na kuandika habari zinazokosoa utawala.
Si hivyo tuu miezi kadhaa iliyopita , kumekuwa na matukio ya kuuawa na kupotea kwa wanasheria yaliyofuatiwa na mgomo mkuwa wa madaktari nchini humo , matukio ambayo Serikali ya Rais Kenyatta imekuwa ikinyoshewa vidole.
Na baadaye serikali imekuwa ikipinga vyama kuwa na vituo vya kujumlisha matokeo kitu ambacho chama chetu cha upinzani nchini kinaamini na kutuaminisha watanzania ni moja ya sababu ya kukosa ushindi kwenye uchaguzi mkuu uliopita.
Je, CHADEMA haioni kama inamuunga mkono mtu ambaye anafanya kitu ambacho hata nchini inapigania kisiwepo?
Au ni lazima kupingana na kile ambacho Rais Magufuli anaoneka akukipenda?
Haioni kama kumuunga mkono mmoja wa wagombea Urais tena kwa tamko Rasmi la Chama kutaleta mngongano wa kidiplomasia kama upande iliouchagua ukashinda?
Na Je, haioni umuhimu wa kuaachia Wakenya wamchague Rais wao , na kusubiri kumpongeza mshindi aliyeshinda kwa haki?
Kwa upande wa Chama Cha Mapinduzi, licha ya kutokuwa na tamko Rasmi laChama  imekuwa ikisemwa huku na kule mitandaoni kuwa wanamuunga mkono Mgombea wa Upinzani Ndugu Raila Odinga  kwa kuwa tu ana urafiki wa muda mrefu na Mweyekiti wa chama chao ambaye ni Rais wa Jamuhuri.
Nao hawaoni si sahihi kuwaachia Wakenya waamue na kumpongeza Mshindi?
Hawaoni kama wanaharibu diplomasia ya nchi  zetu kama wampingae akashinda Urais?
Kupitia Kalamu Yangu nashauri CHADEMA na CCM kusubiri kuwapongeza washindi.
Alamsik.

0 comments:

Post a Comment