ads

Monday 5 June 2017

DIAMOND PLATNUMZ HAPITI NJIA ZA FEROUZ


Na. Mwanakalamu
Kwa kifupi katika harakati za kufikia na mafanikio hasa kwa kutumia sanaa washauri ni msaada mkubwa ni wale jamaa "Masela" ambao ukaribu wako na wao unawafanya wajitoe kwa hiari ama kwa kusukumwa na mazingira.
Unapofanikiwa wale jamaa wanakuwa na mategemeo makubwa ya kusaidiwa na wewe wengine wanataka pesa wengine watajidai wana vipaji vyenye uhusiano na sanaa yako ili tuu wapate mchongo...mfano kama wewe mwanamuziki atajidai ni Dj ili mwende sambamba kwa kuwa hana utaalamu na weledi wa kazi hiyo mambo mengi yataenda kisela na kukosa ubunifu mwishowe mwanamuziki huanguka.
Pia kundi hilo la masela usipolipa nafasi na kuangalia vigezo vya kitaa yaani achana na akina 'nanii' pale Tandale eti uwe na Sallam hawataki na hapo vita huanza kwa kuwa wanajua maisha yako ya nyuma na udhaifu wako basi watatumia kama fimbo kukunyong'onyesha na usipokuwa makini unaporomoka kabisa.
Diamond ni mfano mzuri wa watu walioamua kuacha taaluma na vipaji vifanye kazi na si usela na kujuana...
Ndiyo maana tulisikia hili na lile kumuhusu mengine ni kweli lakini waliokuwa wakimfahamu ndiyo waliopeleka kwa wale waliokuwa wakihisi ni maadui wa Diamond na kutumia kama fimbo.
Hii ilipelekea Diamond kurushiwa mayai viza kwenye show na mengineyo yote ni Diamond aliyakabili na sahizi anatumia mafanikio yake kuwajibu.
Ndiyo maana nacheka sana watu wanaposema ana 'show off za kipuuzi' kumbe hawajui nani anamkomoa kupooza yale machungu.Wengi hudhani Diamond kila akitupa dongo lamuhusu Kiba ,Diamond ana anaowalenga na ukiona kamlenga Kiba basi ni kwa ajili ya kukukuza bifu kwa ajili ya biashara yake.
Hivyo kuhit na kupotea huweza kuwa kwa sababu hizo.Lakini kuna wale wanaoridhika na kubweteka kama Sam wa Ukweli ambao walipopata yale mahitaji Muhimu waliyokuwa wakiyaota hawana ule uhitaji wa kutamani zaidi..mfano unatamani kuwa na pikipiki ukiipata hutamani tena gari ama gari zuri unarudi ulikotoka ukifurahia 'Kifekon' Chako.
Uvivu na ujinga ni sababu, yaani mtu anakuwa tuu mvivu matokeo yake lazima uishiwe.Pia kuna athari za kutumia madawa ya kulevya kwa 'kiwango kilichopitiliza' nimesema kwa kiwango kilichopitiliza kwani wanamuziki wengi pengine huwa na tabia ya kuyatumia madawa hayo wakiwa na pesa hupata uhakika wa kuyapata hivyo hupitiliza kile kiwango chao cha awali wakija kufilisika hawawezi kumudu tena kiwango hicho.
Pia wapo wanaohit tuu kama bahati... Mfano Chellea man na Baba levo

0 comments:

Post a Comment