Na. Steven Mwakyusa (Mtu makini)
Mara nyingi huwa nikitaka kupata burudani ya Rhymes katika muziki wa bongo fleva, wazo la kwanza huwa linanijia kumsikiliza Afande Sele! Huyu jamaa alikuwa na namna yake ya uandishi yenye kufurahisha sana, alikuwa anaonya, anakemea, anajisifu, anajitukuza na akiamua kusifia anasifia japo ni mara chache sana!
Mayowe ndiyo track iliyomuweka kwenye ramani kama Solo artist japo alishaimba nyimbo nyingi tu akiwa na Sugu, huku kibao chake cha Afande Anasema kikiishia kwenye album ya Sugu(Milenia) kwani hakikupelekwa redioni!