Na. Mwanakalamu
Asubuhi ya tarehe tisa April mwaka 2012 Tanzania na Afrika kwa ujumla iliamka na taarifa ya kifo cha aliyekuwa gwiji wa filamu nchini Marehemu Steven Kanumba.Ilikuwa ni taarifa iliyoshtusha na kuumiza watu wengi sana.Kwanza kutokana na sababu iliyopelekea mauti ya kijana huyo aliyekuwa mchapakazi wa kiwango cha juu ambayo ilimhusisha nyota mwingine wa filamu Binti wa Mzee Michael maarufu kama Lulu, pia mauti kumkuta kijana huyo akiwa kwenye kiwango cha juu kabisa cha mafanikio katika kazi zake.





