ads
Showing posts with label Juma Kaseja. Show all posts
Showing posts with label Juma Kaseja. Show all posts

Sunday, 15 May 2016

KASEJA TAJIRI ANAYEIDAKIA MBEYA CITY –MWISHO



Na.Mwanakalamu
Katika sehemu iliyopita  tuliishia pale nilipopata taarifa za kutoka katika kile kijiji cha Kaseja mtoto lakini  kuna kitu nilichomwahidi yule mtoto na kumfanya afurahi sana.
Ni kitu gani hicho?  Tuendelee na simulizi hii ya kuvutia.
Baada ya kuzunguka huku na huko katika siku ile  iliyokuwa ya mwisho katika ziara yangu  nikiwa na yule rafiki yangu nilifanilkiwa kugundua mambo mengi sana.Katika niliyokuwa nimeyagundua ni majina ya wachezaji wachache sana wa Tanzania yaliyoikuwa yakisikia midomoni mwa  watoto lakini mwengi yalikuwa ni majina ya wachezaji wa Ulaya na Amerika.
Palikuwa na akina Messi, Rooney, Mata, Ronaldo na wengine wengi huku majina machache kama Kaseja, Mwameja,Tegete, Ngasa na mganda Okwi.Lakini kulikuwa na kitu cha ajabu kidogo kwani fualana nyingi za timu za nh’ambo zilikuwa na majina na namba za wachezaji wakati wale waliokuwa wamejiita majina ya wachezaji wa Tanzania walikuwa  ama wameaandika kwa rangi za nyumba ama wamechora kwa wino wa peni  au walikuwa hawajaandika chochote.
Ilinisikitisha sana, lakini sikuwa na namna zaidi ya kuamini kuna siku nitatumia kalamu kuufikisha ujumbe wangu kwa matajiri hao wakitanzania waliokuwa wakiziacha fedha zikiishia kwenye mitumba kutoka Ulaya iliyopitia Malawi na Msumbiji.
Siku iliyofuata nilisafiri kwa pikipiki hadi nilipofika kwenye mji ambapo palikuwa na gari zilizonifikisha Mjini Songea ambapo kitu cha kwanza nilichokifanya ni kutimiza ahadi yangu kwa Kaseja Mdogo.Niliingia kwenye duka moja la vifaa vya michezo ambapo nilipata kununua raba za michezo za saizi ndogo ,bukta na fulana nyekundu na nyepe kasha nikaingia mtaani kwa wataalamu wa nembo na michoro ya nguo ambapo niliwaeleza waaandioke namba moja na jina la Juma Kaseja Mgongoni.
Yule jamaa aliniangalia usoni na kuanza kufanya kazi niliyokuwa nimemweleza huku akionekana kutaka kuongea kitu lakini alionekana kama kuniogopa hivi.
‘’Vipi mbona kama kuna kitu unataka kuongea?’’ Niliamua kumuuliza.
‘’Hivi unajua Kaseja anachezea mbeya City?’’ Alinijibu kwa swali.
‘’Naaam nalijua hilo’’
‘’Mbona umemnunulia jezi ya Msimbazi?’’
‘’Kaseja ni Simba na Simba ni Kaseja’’Nilimjibu.
‘’Hiyo ilikuwa zamani  siyo leo’’Aliongea kama akinikosoa vile.
‘’Hapa hadi leo kaseja ni Simba sema Simba hawataki iwe hivyo,Masabiki tunatamani hata awe mshauri wa timu hata kama hachezi, iwe tuu kama Drogba alivyorudio pale chelesea ama anavyofanya Mgosi pale Msimbazi’’Nilieleza kwa masikitiko kidogo.
‘’Lakini si kwa viongozi wale , viongozi waliamua kumwacha kisa tuu yeye ni maarufu na tajiri kuliko wao’’Ananidokezea kitu huyun jamaa huku akionekana kuachana na ile kazi ya kuchora a,anaonekana mwenye hasira.
‘’Kwa hiyo Kaseja ni tajiri sana?’’ Namuuliza nikiwa siamini kauli yake.
‘’Ndiyo ni tajiri na anaweza kuwa tajiri zaidi’’
‘’Kivipi?’’
‘’Unaambiwa Kaseja ana miradi mingi kawekeza huko , lakini bado ananafasi ya kuwa tajiri’’Ananieleza yule jamaa wakati huu anaendelea kuchora.
‘’Kivipi?’’Nalirudia swali langu.
‘’Unajua hapa ulivyonunua hii jezi na kuja kuichora kwangu , hela hii ilikuwa yake ila hajaamua kuwekeza huku’’
‘’Ila kweli’’Najibun na kusubiri aongee inaonekana ana mengi sana.
‘’Unaona hii?’’ Ananiuliza akinionesha kitu kwenye simu yake.
Ni video iliyowekwa na Kaseja kwenye ukurasa wake wa instagram , inamwonesha akishuka kwenye basi huku akishangiliwa na kundi kubwa la watoto na vijana.Hapo ananikumbusha siku moja alipokuja na timu yake ya Simba  mwaka 2010 pale Njombe ambapo watoto wato walianza kumshangilia  tangu aliposhuka kwenye basi, pale hotelini walipolala wachezaji watoto walikuwa hawabanduki wakimchungulia Kaseja wakiita jina lake, kumbuka kipindi hicho Simba ilikuwa pia na akina Okwi sijui Mgosi lakini Kaseja alikuwa kivutio cha kila mtu.
Uwanjani pale Sabasaba ingawa hakuanza kucheza watoto walikuwa kwa kaseja tuu si kwa timu iliyokuwa uwanjani.
‘’Hiyo ilikuwa Shinyanga, kila apitapo hali inakuwa hivyo, Kaseja ana nyota ya akina Diamond, Lowasa na Alikiba’’Ananieleza yule jamaa baada ya kunionesha picha kadhaa za kaseja alizokuwa ameweka kwenya akaunti yake.
Lakini alinionesha picha moja ambayo iliniumiza moyo wangu ,ilikuwa ni picha iliyomwonesha akiwa uwanja wa Taifa akishangilia kipindi hicho yupo Simba, chini yake kuna maandishi.
‘’WANASIMBA MNIKUMBUKE KWA MABAYA YANGU’’
Hiyo ilikuwa pia ni komenti ya picha iliyokuwa imetangulia baada ya dada mmoja kumwambia anatamani arudi Msimbazi, huyo dada alidai kuwa amekuwa shabiki wa Simba kwa sababu yake hivyo hata haoni umuhimu wa kuwa  Simba, alkini Kaseja alimjibu huyo dada kuwa yeye na wanasimba wenzake wamkumbuke kwa mabaya yake.Iliumiza kweli kipenzi huyu wa Simba aliyaongea ya moyoni mwake , ilionesha wazi kuna kitu hakikuwa sawa katika kuondoka kwake msimbazi ingawa anaonekana kuwa na mapenzi mema na timu hiyo.
‘’Hii ndo Tanzania’’Niliongea kwa kifupi.
‘’Lakini ana nafasi’’ yule jamaa ananiambia kwa kifupi akiiweka vizuriile fulana ambayo alikuwa amemaliza kuichora.
‘’Kurudi Simba?’’Nauliza nikiwa nimehamaki.
‘’Hapana sahizi mkataba wake na Mbeye City umeshaisha tangu muda sasa, lakini aliamua kuitumikia timu hadi  mwisho wa msimu, anaweza kuongeza mkataba ama kwenda timu nyingine na hata akikosa timu anaweza kuendelea na soka akiwa kama mkufunzi ama mhamasishaji  wa wanasoka chipukizi.
 Makampuni yapo mengi awashawishi tuu wanaweka mpunga na kuanzisha kakituo kakizushi kanakuwa ni chuo cha kuwanoa makipa ambao watakuja kuisaidia nchi na hata kuuzwa nje, haijalishi hata kama yeye hatowafundisha yeye waletwe tuu wataalamu wamsaidie huku akizunguka nchi zima mkoa kwa mkoa, wilaya kwa wilaya, tarafa kwa tarafa kata kwa kwata na kijiji kwa kijiji.
Hapo anaenda kutafuta wataalamu na wabunifu wanabuni jezi rangi na muundo wake zinaandiokwa jina lake, anaweka sokoni viatu , gloves na vifaa vingine vya michezo kasha anapozunguka kutafuta vipaji basi huko pia anaweka vituo vyake ambako vifaa vyake vitauzwa huko.
Nakwambia Kaseja ni tajiri mkubwa sana hata asipocheza soka, na katika soko ukiachana na bidhaa za urembo wa wanawake vitu vya watoto vinanunulika sana angalia hata we mwqenyewe umeamua kumnunulia mwanao nadhani baada ya kukusumbua, watoto wakiona watakulilia mzazi na kama nawe hueleweki mtoto anaweza kuiba akaipate jezi full ya Kaeja Tanzania One , Tajiri anayedakia Mbeya City’’.
Anamaliza yule jamaa akinikabidhi jezi zangu ambazo nziweka kwqenye mfuko na kwenda kumpa rafiki yangu mwenyeji wa kule kijiijini mwambao wa ziwa nikimwomba amfikishie rafiki yangu Kaseja mdogo.
Kuna kitu nakikumbuka , naamchelewesha tena yule mwenyeji wangu kwa kuingia palipo na huduma ya intaneti naishusha picha kadhaa za Juma Kaseja na kuzichapa kwenye karatasi naiweka kwenye bahasha na kwenda kuunganisha na ule mzigo wa jezi.
Ninaagana na rafiki yangu kasha naenda uwanja mdogo wa ndege na kufanya taratibu za safari na baada ya saa chache najikuta nipo kwenye jiji la joto , jiji lenye timu ambayo Kaseja ameitumia kwa muongo mzima.
Dah! Huyu ndiye Kaseja tajiri anayedakia Mbeya City.
Niandikie maoni yako hapa  chini.

Friday, 6 May 2016

JUMA KASEJA ''TAJIRI ANAYEDAKIA MBEYA CITY'' 03

Na;Mwanakalamu
Kwanza napenda nikuombe radhi mpenzi msomaji wa makala hii kumuhusu Tanzania One Juma Kaseja kwa kushindwa kuwa nanyi kwa siku mbili mfululizo.Palikuwa na tatizo la kiufundi hivyo nikashidwa kuwaletea uhondo.Katika sehemu iliyopita tuliishia pale nilipokuwa na Kaseja mdogo kule ziwani tumekaa mchangani,Tuendelee.
Baada ya kukaa pale mchangani tukiangalia mazingira ya pale ufukweni kwa muda huku kila mtu akiwa na lake kichwani mwake , nikapata cha kuongea.
''Hivi kama nataka kuoga nitaenda kuoga wapi wakati pana watu kibao?''
''Hapa wamegawa kwa wavulana na wasichana, unaona wale akina mama? pale wanaoga wanawake na hapa tulipo ni sehemu ya kuoga wanaume , wamegawa hivi hivi ufukwe mzima''Alieleza Kaseja mdogo.
''Sawa , ila mbona hapa kuna wakawake pia?''Niliuliza.
''Hapa pana wasichana pia kwa kuwa wavuvi wanakuja na samaki hivyo huja kununua samaki pia hata kama mtu atataka kuoga anakuwa amevaa bukta''Hapo nikafungua tena akili huku nikijiuliza kama nitaweza kuoga ziwani kwa muda wote nitakao kuwa pale kijini.
''Sawa nimekuelewa Kaseja wangu, kwa hiyo huwa unakuja kufanya mazoezi ya kudaka huku?''
'' Mie nadaka pale uwanjani huku kwenye mchanga watu waoga ndo hujifunzia huku mie najifunzia kwenye jamvi la uwanja wa taifa''Anajigamba  mtoto.
''Kwa hiyo uwanja wenu una kapeti/jamvi kabisa?'' Nauliza kinafiki lakini kabla ya kunijibu anainuka na kukimbilia mahali ambapop wengi wanakimbilia, kumbe wavuvi wamekuja kutoka kuvua watu wnakimbilia mgao naona kundi kubwa la watu wameshika mtumbwi ambao nilihisi ulihitaji watu wanne tuu kuuweka ufukweni.
Baada ya dakika kama kumi hivi Kaseja mdogo anakuja na samaki mkononi na ananishawishi tuelekee nyumbani akanitengenezee samaki wale nile.
Tukiwa njiani Kaseja mdogo ananieleza mambo mengi juu ya watoto wenzake wanaopenda kudaka na wanajiita Kaseja ila anaamini hakuna wa kumfikia yeye ambaye ni mrithi halisi wa Kaseja Tanzania one.
Namtazama usoni kumsoma bila mwenyewe kugundua , anaonekana kuwa makini na alichokuwa anakiongea , aliamini alichokisema ambacho bila shaka yoyote kilitoka moyoni mwake maana alikisema kwa ari kubwa sana.
Moyo wangu ukaumia baada ya kufikiria kama ataingia kwenye kundi la watoto na vijana wengi waliojaribu kuwa kama Kaseja katoka kila mkoa nchini, kila wilaya, kila kata, kila kijiji ama hata mtaa ni mamia ya watoto lakini wanishia kudaka kwenye mabonanza yanayoandaliwa na wanasiasa  karibu na kipindi cha uchaguzi.Ni mamia ya watoto lakini wengi wanaishia kuwa maarufu mitaani mwao umaarufu unaopelekea kupewa ofa za pombe ama wanawake pale wanapofanikiwa kudaka vyema.
Lakini nilimfikiria tena Kaseja Tanzania one anayedakia Mbeya City, ana historia yenye mikasa mingi ambayo kwa mpenda soka halisi lazima umuumize.Kaseja ambaye amewafanya wengi kupenda kudaka, amewafanya wengi kufuatilia soka, Kaseja aliyewafanya hata wasichana ambao soka si kitu wanachokipenda lakini wakajikuta wakipenda soka ili tuu kumtazama, Kasejahalisi ambaye amefanya maelfu ya watu kuishabikia klabu ya Simba , Kaseja aliyewaliza watu wa simba pale alipohamia Yanga lakini alifanikiwa kupewa heshima ya mashabiki hata alipokuwa upande wa pili.Kaseja ambaye hata watoto wasiowahi kumwona wanaliimba jina lake,Kaseja golikipa ambaye anaingia kwenye rekodi za kuwa  katika kundi dogo la wachezaji waliodumu kwenye soka kwenye kipindi kirefu.
Ndiyo Kaseja aliyetemwa na Simba kienyeji licha ya kuitumikia kwa zaidi ya miaka saba, ndiyo ni huyo huyo huyo ambaye leo hii kuna viongozi wa soka wanatamani wapenda soka tumsahau kwa nguvu , tuusahau na mchango wake kwenye soka la Bongo ama Afrika mashariki kwa Ujumla kwa kuwa tuu  hajawai kuleta tunzo ya uchezaji bora Afrika ndiyo ni huyo ambaye leo hii kuna mtoto ambaye anatamani kuwa kama yeye licha ya kutomwona.
Tunafika nyumbani hapo nakutana na taarifa inayonitaka niondoke siku inayofuata kurudi jijini Dar es salaam , taarifa ambayo inamfanya hata Kaseja mdogo asikitike.
Lakini namwahidi kitu ambacho kinamfanya arukeruke kwa furaha.
Ni kitu kani hicho?
TUKUTANE KESHO AMBAPO TUTAMALIZIA SIMULIZI HII YA KASEJA NA KUNZA NYINGINE ITAKAYOMUHUSU AMIS TAMBWE.

Tuesday, 3 May 2016

JUMA KASEJA ''TAJIRI ANAYEIDAKIA MBEYA CITY'' 02

Na;Mwanakalamu
Sehemu iliyopita ya simulizi hii tuliishia pale Kaseja mdogo kutoka katika kijiji hichi kilicho kando kando ya ziwa Nyasa upande wa Tanzania aliyekuja na kipande cha gazeti moja la michezo nchini Malawi chenye picha ya Juma Kaseja,tuendelee na simulizi hii ya kusisimua.
Nilimtazama yule mtoto kwa huruma kwani nilihisi  redio ni kitu pekee kilichomfanya akawa na mahaba ya dhati kwa mwanamichezo huyu nguli nchini.Nilimhurumia pale nilipofikiri kama Maji maji itashuka daraja , nafasi yake ya kumwona Juma Kaseja ingekuwa ndogo sana katika maisha yake.Pia nilifikiria kama Juma Kaseja baada ya kumaliza mkataba wake pale Mbeya City ataenda timu gani? 
Atarudi Dar es Salaam? 
Ataongeza Mkataba Mbeya City?
Atakuwa wapi?
Nikamshukuru yule mtoto  kwa kifungua kinywa chake alichonipa na kumuuliza kama ataweza kunipelekea ziwani ili nami nikalishangae tena luile ziwa nililokuwa nimekaa juu yake kwa siku kadhaa nikiwa na hofu kuu.
Akiwa na furaha alikubali kunipeleka, kwa kuwa ilikuwa Jumamosi watoto wengi walikuwa mitaani wakienda na kurudi kutoka ziwani na ndoo kichwani, samaki mkononi.
''Mbona kila anayetoka ziwani anarudi na samaki?''Namuuliza rafiki yangu mpya nikiachana kabisa na mwenyeji wangu ambaye alikuwa shuleni.
''Wamewanunua wengine wanapewa tuu, kama yule pale kapewa''Anaongea akimwonesha mama mmoja aliyekuwa na rundo la samaki wabichi mikononi.
''Umejuaje?''
''Nimejua kwa kuwa samaki wale si wa kununua wale unapewa tuu''
''Kwa hiyo hata sie tutapewa?''
''Ndiyo tukikuta wanatoka kuvua tutapewa na wewe mgeni ndo utajaziwa''
'Ila naona aibu kuomba''Naongea nikimtazama usoni yule rafiki.
''Usijali wakiniona nipo na wewe halafu nikaenda utaona maajabu ya kaseja kufunga magoli''Alijigamba akimalizia na kicheko.
''Kaseja si golikipa atafungaje magoli?''Namuuliza kwa kumtega.
''Aliwafunga Yanga kwa penati kipindi cha marehemu Mafisango siku ile ya tano bila, pia akiwa Yanga aliwahi kufunga magoli mawili kama sikosei pia alitoa pasi ya goli siku ile Okwi alipofunga dhidi ya waarabu kwenye ule usiku wa maajabu tulipotia kitumbua mchanga''Ananikumbusha mengi juu ya umahiri wa Juma Kaseja na kuniacha mdomo wazi.
''Lakini pia alikosa penati kule Sudan''Namkumbusha.
''Nakumbuka achana na kukosa penati yule jamaa anadaka sana penati , kama nifanyavyo mie''Ananikumbusha hilo rafiki yangu huyo.
''Naaam huyo ndiye Juma Kaseja'' Naongea wakati huo tulikuwa tumeshafika ziwani tunaamua kukaa kwenye mchanga ufukweni.
Tukutane kesho katika kisa hiki cha kweli kumuhusu Tanzania one aliyebaki kwenye soka.