Monday, 16 February 2026
Darasa anapotupa 'darasa'
MABIBI NA MABWANA, NAMLETA KWENU CESC FABREGAS
UFUNDI WA MESUIT OZIL
Tuesday, 21 November 2023
BASI
Basi.
KAMA NINGEKUWA JUA
SIKU ZA UJANA WA DIEGO COSTA
Na. Kenny Anjelina
HAPO ZAMANI ZA KALE
JINSI AMBAVYO RAIOLA ANGEISUMBUA DUNIA KWA MBAPPE
KIBURI KINAVYOWAUA WAJERUMANI
Na. Kenny Anjelina
Waingereza wanamsemo wao, Curiosity killed a cat. Yaani udadisi mwingi ulimuua paka. Paka hudadisi hata vitu vinavyomzidi uwezo mwisho hupata madhara na hata kufa.
July 13, 2014, usiku ule Wajerumani walikuwa na furaha sana. Unajua kwanini? Walikuwa wanatwaa taji la Kombe la Dunia, tena njiani wakitoka kutoa semina elekezi kwa Brazil, palepale kwao waliwapa 1-7. Raha iliyoje?
Nafikiri usiku ule pale Rio de Janeiro ndo tulimaliza ubora wa Ujerumani. Tangu hapo hatujaona hata robo ya mafanikio ya ubora wa Ujerumani ile.
Mwaka 2018 waliishia hatua ya makundi pale kwa Vladimir. Walishindwa kufurukuta mbele ya Korea kusini na wahuni Mexico. Bingwa mtetezi, akatolewa hatua ya makundi.
Watu wa mpira walihisi ni bahati mbaya tu. Lakini kilichojirudia mwaka 2022, pale Qatar, kutolewa tena kwenye makundi tukajua tu Ujerumani imeanguka.
Dunia nzima inajua Ujerumani imeisha lakini wao tu pekee ndo hawaamini kama wameisha. Wana kiburi, ndo kinachowaua.
Baada ya Qatar, wakacheza mechi nyingi ambazo zinawapalia kila siku. Lakini hawataki kuanza upya, wanaamini wao bado wapo timamu.
Mpira umebadilika, umetoka kwenye matumizi ya nguvu na kucheza kwa nafasi hadi kwenye matumizi ya sayansi ya mchezo na kutimiza majukumu ya pamoja.
Uingereza, Ufaransa na Uholanzi wapo huko. Argentina ndo tusiseme, unaona jinsi Rodrigo De Paul anavyohaha uwanja mzima. Hakuna matozi tena.
Ila Ujerumani wao bado wanaamini katika nguvu na kupishana. Bahati mbaya wana Gundogan na Musiala ambao hawawezi kutumia mabavu.
Juzi walijaribu kuacha kiburi chao, wakaamua kuiga sayansi kwa kumchezesha Kai Havertz kama mlinzi wa kushoto lakini wakawa wamechelewa, wakafa 3-2 kwa Uturuki.
Ujerumani inabidi wakubali kwamba kizazi cha dhahabu kimeisha, inabidi waanze chini. Kama Uingereza na Uholanzi walivyofanya.
Wakiendelea na udadisi wao watakufa kama ambavyo Italia. Wamekosa michuano miwili ya kombe la Dunia mfulululizo na juzi ilibaki kidogo washindwe kufuzu Euro
DAR NA WATU WAKE
Thursday, 12 January 2023
WHEN THE STORM COMES
Whether it's a rain storm,
I will take off my coat,
hide you like a tent,
When the storm comes, I will protect you my love.
I will protect you, dear,
in words and actions,
Importantly, I will love you,
When the storm comes, it will not bother you.
It will find me strong,
and fulfill the duty,
The duty of a good father,
A responsible father,
And a wise husband,
When the storm comes, I will keep you safe.
I will keep you safe,
give you the victory,
The nonsense will stop,
When the storm comes, I will be your shield.
I will be your shield,
you and our children,
I don't waver here and there,
betrayal is not a personality,
When the storm comes, believe that you are safe.
Believe you are safe,
safe heart and body,
You will remain a mother,
I will not stop working,
whenever I get a deal,
When the storm comes, it will find us strong













