ads
Showing posts with label Anza Mwaka. Show all posts
Showing posts with label Anza Mwaka. Show all posts

Monday, 9 January 2023

HIS HYPOCRITIC SONG


 

It's a catchy song, anyone with an ear,

Those who sing to him, who love his coming,

And it's a lie for them, , 

He is finished, with his own songs, 

He will make you laugh, turn around and scream, 

Always the victim.


If there is a black one, the bets crush the white one, 

If he is on the bus, let's be afraid of the plane,

Today he will crush a pumpkin, tomorrow he will praise it, 

Call the hill a park, if you want to run,

When the rain comes, he will praise the sun.


What he will praise, let us see the soothsayer, 

And pretending to be giving you a secret.

His reputation is to forget, he is a champion of ignoring, 

He does not want to lower the stake, if the truth informs him, 

We will not see scorners, claiming you are lying, 

His hypocrite song, this never stops. 



If you want to sing with him, don't raise your voice, 

Also give up your mind, let him monopolize it,

Lies to honey, others to hurt,

Let me tell you one thing, 

Do the trick, avoid him immediately, 

His hypocrite song, this never stops.

Thursday, 28 April 2022

UNAPOMPATA MWANA

 














Waweza hisi waota,kuwa umepata mwana,

Kutwa mwili utatota,na mawazo kugongana,

Huku na huko kugota,kumbe walisaka jina,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Miezi ya kutazama,kama hukuiamini,

Yale machungu ya mama,kama hukuyaamini,

Mawio hadi kuzama,mama yupo taabani,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Ulishapanga na jina,ghafla linakupotea,

Lile waona hapana,na jinsi ulikosea,

Kumbe halina maana,ndivyo unajitetea,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Nawe waweza akiba,mwana aje kutumia,

Hujiwazii kushiba,yeye wamfikiria,

Wala huhofu shuruba,mwana wamtafutia,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Mkeo utamjali,nawe sasa unapika,

Waijali yake hali,wafua na kuanika,

Hutaki aende mbali,ili asije kuchoka,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Sasa wapokea simu,za wakwe na ndugu zako,

Maadili ni muhimu,umekua wimbo wako,

Ratiba zako si ngumu,wajiwekea miiko,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Waitwa baba fulani,jina lako lafifia,

Simu za akina Jeni,sasa unazichunia,

Wawahi na ibadani,swala unazingatia,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Atafanya kazi gani,kabwela unakisia,

Hata akiwa shambani,siyo jasho kutumia,

Wapenda awe rubani,ndotoyo isotimia,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Mwana kipata mafua,utahaha siku nzima,

Kucha utaliga dua,kumuombea uzima,

Tafikia kuagua,mwana imtoke homa,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Kipata hela ya nyama,husiti kuinunua,

Utaiandaa sima,hata kwa moto wa bua,

Utahimiza kusoma,mwanao atapokua,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Siku utazihesabu,lini mwana katembea,

Taweka kwenye vitabu,siku atayoongea,

Humwazii kuwa bubu,mwana utamuombea,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


Utawaza kuwa baba,na mume aliye bora,

Utamwepusha shuruba,kumkwepesha bakora,

Tamganda kama ruba,na kumpa masikhara,

Unapompata mwana,kabwela wahangaika.


#kaulizamakabwela

Friday, 1 January 2016

MAMBO MATANO YA KUFANYA UNAPOKUTANA NA MPENZI WAKO WA ZAMANI (EX)


Na.Tumsifu Kaoza
1.KUWA MUWAZI. 
Kama upo tayari kuongea na ex wako mkikutana, akuulizapo swali lolote mjibu inavyotakiwa kwa majibu mafupi yasiyo ya kubabaisha yenye ukweli mtupu. Kama ni ndiyo 'ndiyo' na kama ni hapana 'hapana' itakufanya kujenga utu wako na kukupa kujiamini.

2.USIJITONGOZESHE. 
Kama umeshaachana na mpenzi wako mpya kwa sababu ya huyo mpenzi wako wa zamani usifanye mambo ya kujitongozesha kama vile kukaa naye karibu kumchekea chekea au kumtega kwa namna yeyote ile kama ikitokea bado unampenda muache yeye akuanze na umsumbue katika kumjibu kwa sababu kama mlishaachana huna hakika lile kosa halitajirudia mkirudiana.

3.KUWA NA MAWAZO CHANYA. 
Wengi wanapokuwa pamoja na wapenzi wao waliopita hufikiria negative hujiuliza anawaza nini? Ananiona mbaya? Vipi kama anakuja kunionesha mpenzi wake mpya? Haya ni maswali machache yanayowapitia wengi vichwani mwao. Lakini kama ukiwa na mawazo chanaya unaweza kujiamini na uwezo hata wa kumface huyo mpenzi wako aliyepita kwa hiyo uwapo na ex wako fikiria mawazo chanya.

.RELAX. 
Muda mwingi watu mnapokutana na wapenzi wenu waliopita huwa mnapanic kitu ambacho unatakiwa kufanya ni kutulia na kuvuta hewa nyingi ndani na kutoa nje hii hujenga kujiamini na kuondoa hofu iliyojengeka usoni mwako.

5.USIONESHE KUKOSA FURAHA KATIKA PENZI LAKO LA SASA. 
Usimpe nafasi x wako kujiona yeye ni muhimu sana katika maisha yako yaani ajione yeye alikuwa ni furaha yako ya pekee hata kama huyu wa sasa hana tofauti na yeye lakini jitahidi kujiweka sawa na kumuonehsa kuwa hakuna tatizo huyu wa zamani ili kujenga kujiamini kwako kila mnapozungumzia habari za mahusiano.
Heri ya Mwaka Mpya.