ads
Showing posts with label Funga mwaka. Show all posts
Showing posts with label Funga mwaka. Show all posts

Friday, 1 January 2016

KALAMU YANGU 'YAPATA MTOTO' MWAKA MPYA


Ni siku ya furaha kwa kila mwanadamu kuuona mwaka mpya, wengi walitamani kuuona huu mwaka lakini wameshindwa kuuona huku malengo yao mengi juu ya mwaka huu  yakizikwa bila kutimia hata kujaribiwa.
Naam ni mwaka mpya kila mtu anaupenda kama matatizo yatakuja basi tunajua ni kawaida kwa kiumbe yoyote kukutana na matatizo anapopambana na mazingira katika kupata mahitaji yaliyo muhimu na yale yasiyo ya muhimu.
Kalamu yangu inawapongeza wote walioufikia huu mwaka na tunawapa POLE wote waliowapoteza wapendwa wake mwaka uliopita.Pia tunampongeza mwanakamu Mwenzetu Steven Mwakyusa ambaye anatimiza miaka kadhaa tangu azaliwe kule kwetu mtoto huyu tungemwita 'Mwaka' ila wacha tumwite Steven Mwakyusa Mtu makini kama apendavyo kuitwa.

HONGERA   KAKA STEVEN MWAKYUSA MUNGU AKUONGEZEE HEKIMA NA BUSARA NA MIAKA MINGI YA KUISHI YENYE BARAKA ZAKE.

Wednesday, 30 December 2015

NYIMBO 20 ZA BONGO FLEVA ZILIZOFANYA VIZURI 2015,VANESSA MDEE 'KIBOKO'

Imeandaliwa na; Steven Mwakyusa,Tumsifu Kaoza na Moringe Jonasy
Hizi ndizo nyimbo zilizofanya vizuri zaidi katika bongo flava kwa mwaka 2015
1. Nivumilie-Barakah da Prince & Ruby

2. Subira-Kassim Mganga & Christian Bella

3. Sophia-Ben Paul 

4.Nashindwa- Christian Bella 

5. No body but me-Vanessa Mdee &Kcee

6. Chekecha Cheketua-Alikiba 

7. Na yule-Ruby

8. Game-Navy Kenzo ft Vanessa Mdee

9. Nana-Diamond & Flavour

10. Shauri zao-Belle 9

11. Nikuite nani-Jux

12. Suna-Barnaba

13. Nitazoea-Mo music

14. Nusu nusu-Joh Makini

15. For u-Q chilla

16. Shikorobo-Shetta

17. Viva Roma- ROMA

18. Safari-Nick wa pili, G nako, Joh Makini & Vanessa Mdee

19. Siri-Barnaba & Vannesa Mdee

20. Aiyola-Harmonize

Hawa wameonekana kufanya  vizuri kwa mwaka unaoenda kuisha, ukiangalia kwa makini katika hii list utagundua kwamba kuna aina ya muziki ambayo inashika chart kwa sasa..na si nyingine bali ni Afro-pop!!
Ukimwangalia Shetta kabadilika kwa kiasi kikubwa, Q chilla naye alionesha mabadiliko makubwa katika ngoma ya For u, huku naye Jaffarai akijaribu kutoka katika stail yake ya zamani katika wimbo aliomshirikisha Kassim "Wakati"...ni wengine wamejaribu kuendana na wakati uliopo, pengine bahati haikuwa kwao!!
Ukiangalia nafasi ya Hip hop na RnB bado ni finyu, huu unaonekana kuwa muziki ambao unapoteza mvuto kila kukicha...wasanii wengi wameshindwa kutamba licha ya kutoa nyimbo..katika hilo kundi wamo akina Young D, Jos Mtambo, N2N pia wasanii wa Tamaduni music!!
Wapo wasanii waliofanya vizuri mwaka uliopita lakini mwaka huu wameshindwa kufurukuta, hawa ni pamoja na Recho, Mwasiti, Tumbulo, Rich Mavoko, Ommy Dimpoz, MwanaFa na Ay, Madee, D knob pia Dayna Nyange kwa kutaja kwa uchache!!
Nyota imeonekana kung'aa sana kwa Vanesa Mdee, Ruby pamoja na Christian Bella...hawa wameweza kutengeneza hits zao...na pia kufanya vizuri pale waliposhirikishwa!!
Mwisho niwapongeze wasanii wote walioweza kutengeneza nyimbo nzuri na kutoa burudani ya uhakika kwa mashabiki, muziki wetu unakua japo bado kuna zile kauli kwamba muziki ulikuwa zamani!! Leo si ajabu kuona nyimbo zetu zikichezwa katika radio stations na Tvs za mataifa mbalimbali! 
Bado naamini tunaweza kufanya vizuri zaidi ya hapa na kuitangaza vyema nchi yetu!!

Happy New Year 2016!!