ads

Tuesday, 21 November 2023

BASI













Kaditama nimetua, sisongi sirudi tena,
Mambo nimeyatibua, hata nife hutoguna,
Kweli yote nimejua, ulianza mbali sana,
Basi.
Nilihisi tunaota, kumbe ninajidanganya,
Ilipita myaka sita, sina nililolifanya,
Mwenyewe ukajipata, mwenyewe sikujiponya,
Basi.
Nikaiweka busara, kumbe linaletwa shari,
Kaona kovu imara, kumbe njia ya hatari,
Ninazuia hasira, waniotea kaburi,
Basi.
Kaniundia ubaya, kwote wanone kituko,
Kutwa naijenga kaya, mwenzangu kucha mitoko,
Kila siku kwangu mbaya, kumbe kwako ni ujiko,
Basi.
Kihisi yule adui, kwake utajibagaza,
Nikajifanya sijui, sije wana waumiza,
Nilishajua wewe chui, heri kwangu kunyamaza,
Basi.
Niliposaka suluhu, wapasha vyako viporo,
Kavuka hadi Ruhuhu, Pwani hadi Morogoro,
Kumbe umeshakubuhu, mie kunipa kasoro,
Basi.
Umeutibua moyo, akili na wangu mwili,
Heri un'one na choyo, naipamba yangu hali,
Sasa ninatoka mbiyo, nikusanye zangu mali,
Basi.
Basi sasa imetosha, yote nimeyakubali,
Basi sasa yamekwisha, sasa ninakwenda mbali,
Basi sitokukumbusha, zile ahadi za kweli,

Basi. 

1 comments:

  1. Nilimkuta mke wangu akinidanganya baada ya kugundua jumbe kati yake na mpenzi wake wa zamani kwenye simu yake. Nilihuzunika sana kwa sababu sikuweza kuelewa nilichofanya ili kustahili hilo. Nilipomkabili kuhusu hilo, alikasirika na kusema alitaka talaka.

    Nilimpenda sana, na sikuweza kuvumilia wazo la kumpoteza mke wangu na watoto kwa mwanaume mwingine. Kisha nikajulishwa kwa mtu aliyedai kusaidia kufufua mapenzi katika ndoa zenye matatizo.

    Saa chache baada ya Dkt. Dawn kusema amekamilisha uchawi, mke wangu alinipigia simu nilipokuwa kazini, akiniomba nimsamehe na kusema anaomba msamaha kwa kutaka kuondoka kwenye ndoa yetu.

    Nilishtuka kabisa. Machozi yalinitoka mara moja kwa sababu niliamini kweli kwamba nilikuwa nimepoteza familia ambayo nilikuwa nimejitahidi sana kuijenga.

    Ikiwa unapitia matatizo ya uhusiano na unahitaji msaada, unaweza kuwasiliana na Dkt. Dawn kupitia WhatsApp: ( +2349046229159 ). dawnacuna314@gmail.com

    kwa suluhisho la haraka na lenye nguvu.

    Huduma zinazotolewa:
    • Uchawi wa mapenzi
    • Kurejesha upendo na furaha katika mahusiano na ndoa
    • Kuvutia mpenzi mpya
    • Usomaji wa mahusiano
    • Tambiko za bahati nasibu
    • Kurejesha mali iliyoibiwa
    • Mwongozo wa hatua kwa hatua kwa masuala na changamoto za kibinafsi

    ReplyDelete