ads

Tuesday, 21 November 2023

KAMA NINGEKUWA JUA













Huwa halioni wivu, wala kuchukia kitu,
Jua halina uchovu, halibadiliki katu,
Huwa linatunza nguvu, jua si kama msitu,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Jua shahidi wa vingi, wala haliji kusema,
Usiri kwake msingi, halijawahi kugoma,
Iwe mboga iwe bangi, moja hawezi kuchoma,
Heri ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Singetamani usiku, wote mkawa nuruni,
Na nikasirike siku, niwache wiki gizani,
Wacha munone kasuku, mkanitoa thamani,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Mngeona tabasamu, hata nikiwa tabuni,
Mkininyima salamu, isinifike moyoni,
Hata nisiwaze simu, anayepiga ni nani,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Nizipuuze ahadi, mliziweka gizani,
Nisipandishe midadi, mkikana hararani,
Ama kumwona hasidi, akitamba kanisani,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Ugonjwa ningepuuza, na kuikwepa sonona,
Hili linalonunguza, nisingelijali sana,
Kimya ningejiuguza, nikafa hata kupona,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Ningekuwa peke yangu, mwezi na wingu kwa mbali,
Nisingewaza uchungu, nyota siponikubali,
Zaidi ni wangu Mungu, langu pendo astahili,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Singekuwa na wana, nife wakanililia,
Na mke tukagombana, ili aje nikimbia,
Wala kusema hapana, nishindwe kuvumilia,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Nisingemuwaza mama, au baba kumjali,
Huko na huko kusoma, kisha nife kwa ajali,
Mama akashika tama, kuwazia yangu hali,
Kama ningekuwa jua, ningekuwa kitu bora.
Basi hivyo siyo jua, siyo mvua wala nyota,
Macho nitayakodoa, na kusota nitasota,
Nikiumwa naumia, na furaha pia napata,
Kama ningekuwa jua.....

1 comments:

  1. Nilimkuta mke wangu akinidanganya baada ya kugundua jumbe kati yake na mpenzi wake wa zamani kwenye simu yake. Nilihuzunika sana kwa sababu sikuweza kuelewa nilichofanya ili kustahili hilo. Nilipomkabili kuhusu hilo, alikasirika na kusema alitaka talaka.

    Nilimpenda sana, na sikuweza kuvumilia wazo la kumpoteza mke wangu na watoto kwa mwanaume mwingine. Kisha nikajulishwa kwa mtu aliyedai kusaidia kufufua mapenzi katika ndoa zenye matatizo.

    Saa chache baada ya Dkt. Dawn kusema amekamilisha uchawi, mke wangu alinipigia simu nilipokuwa kazini, akiniomba nimsamehe na kusema anaomba msamaha kwa kutaka kuondoka kwenye ndoa yetu.

    Nilishtuka kabisa. Machozi yalinitoka mara moja kwa sababu niliamini kweli kwamba nilikuwa nimepoteza familia ambayo nilikuwa nimejitahidi sana kuijenga.

    Ikiwa unapitia matatizo ya uhusiano na unahitaji msaada, unaweza kuwasiliana na Dkt. Dawn kupitia WhatsApp: ( +2349046229159 ). dawnacuna314@gmail.com

    kwa suluhisho la haraka na lenye nguvu.

    Huduma zinazotolewa:
    • Uchawi wa mapenzi
    • Kurejesha upendo na furaha katika mahusiano na ndoa
    • Kuvutia mpenzi mpya
    • Usomaji wa mahusiano
    • Tambiko za bahati nasibu
    • Kurejesha mali iliyoibiwa
    • Mwongozo wa hatua kwa hatua kwa masuala na changamoto za kibinafsi

    ReplyDelete